top of page

Imeandikwa na daktari wa ULY CLINIC

 

Anozmia

Anozmia ni neno kiswahili lililotokana na neno la kiingereza anosmia ambalo lilitoholewa kutoka neno la kigiriki “osme” lenye maana na nusa na “an” linaloanza ni neno la kizungu linalomaanisha “bila” hivyo neno anozmia linatumika kumaanisa kupoteza uwezo wa kunusa au kutokuwa na uwezo wa kunusa

Baadhi ya maneo mengine yanayotumika ni kama upofu wa kunusa

Anozmia mara zote husababishwa na kuziba kwa tezi za kunusa kutokana na

 

Kupoteza uwezo wa kunusa ni kawaida jinsi mtu anavyozeeka umri,, lakini kuna baadhi ya dawa zinaweza kuongeza au kuharibu uwezo wa kunusa. Sababu zingine zinazoleta tatizo hili zinatokana na kuharibika kwa mishipa ya fahamu inayopitisha taarifa za kunusa kuharibika huku huweza kutokana na kupata ajali mbaya kichwani, maambukizi ya virusi ndani ya kichwa na tiba mionzi kichwani.

 

Magonjwa ya mifumo ya mwili mfano ni ajali ya cerebrovasikula, ugonjwa wa Alzheimer daimenshia, kisonono, saratani ya ubongo na magonjwa ya mfumo wa tezi za endokrini, magonjwa ya lishe na magonjwa ya madhaifu ya mfumo wa fahamu.

 

Muulize daktari wako endapo una dalili hii kwa ushauri, uchunguzi na tiba

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri vipimo na tiba bonyeza hapa au piga namba za simu chini ya tovuti hii

Imeboreshwa 15.11.2020

 

Rejea

  1. Oxford English dictionary

  2. Ulyclinic

bottom of page