top of page

Kupata tiba

Utangulizi

Vihatarishi

Dalili

Vipimo

Matibabu

Homa ya matumbo-Taifodi

​

Imeandikwa na madaktari wa ulyclinic

​

Ugonjwa wa taifodi au homa ya matumbo ni ugonjwa unaodhuru viungo mbalimbali mwilini lakini huanza tumboni, ugonjwa huu husababishwa na bakiteria anaeitwa salmonella typhi na wakati mwingine salmonella paratyphi

 

Vimelea hawa wanapokua kwenye tumbo husafiri kwenye mishipa ya damu na kufika sehemu mbalimbali za mwili kama mifupa, ini bandama, na kisha  huzaliana kwa wingi ndani ya chembe hai nyeupe za damu zinazolinda mwili ilizopo kwenye mifupa, Ini, bandama na mitoki. Mara baada ya kuendelea  kuzaliana katika chembe hizi zinazolinda mwili, chembe hupasuka na bakteria hutolewa kwa wingi na kuvamia maeneo mengi ya mwili na kusabaisha dalili mbalimbali

 

Vimelea wa kusababisha taifodi hutunzwa na binadamu pamoja ambapo wakati huu mtu anakuwa hana dalili zozote za maambukizi. Endapo mbebaji atajisaidia na itakotea kinyesi chake kimechanganyika na maji basi hata maji yanayotumika kuandalia chakula au kunywa endapo hayajachemshwa vyema mtu anaeza kupata maambukizi ya vimelea wa taifodi
 

Ndege pia huwa na vimelea hawa wa taifodi( hasa ndege jamii ya kuku). Mtu anaweza kupata vimelea wa Taifodi endapo atakula mayai mabishi au ambayo hayajachemshwa vema.

​

Vihatarishi, Dalili Vipimo na matibabu

bottom of page