top of page
Kamusi Tiba ya ULY CLINIC

Maumivu kwenye nyonga
Ni hali ambapo mtu hupata maumivu yanayotokea ndani ya eneo la nyonga, yaani sehemu yenye viungo mbalimbali vya ndani kama mfuko wa uzazi, ovari, mirija ya uzazi, kibofu cha mkojo, utumbo na tezi dume kwa wanaume. Aina hii ya maumivu mara nyingi haihusiani moja kwa moja na mifupa ya nyonga, bali hutokana na matatizo ya viungo vilivyomo ndani ya eneo hilo.

Maumivu ya nyonga
Ni hali ambapo mtu hupata maumivu yanayotokana na muundo wa nyonga wenyewe (pevisi), ambao unajumuisha mifupa ya nyonga, viungo vinavyounganisha mifupa hiyo, misuli, tendoni, mishipa ya fahamu na tishu zinazozunguka eneo la nyonga. Maumivu haya mara nyingi huhusiana na mfumo wa mifupa na misuli ya nyonga, badala ya viungo vilivyopo ndani ya eneo la nyonga.
bottom of page


