top of page

Mwandishi:

Mhhariri

ULY CLINIC

Dkt. Benjamin L, MD

Jumanne, 26 Oktoba 2021

Fangasi ukeni kwenye ujauzito

Fangasi ukeni kwenye ujauzito

Maambukizi ya fangasi ukeni ni husababisha kutokwa na uchafu usio wa kawaida wakati wa ujauzito. Tatizo hili huwapata wanawake wengi haswa kwenye kipindi cha pili cha ujauzito yani wiki ya 13 hadi 27 ya ujauzito.


Nini husabaisha maambukizi ya fangasi wakati wa ujauzito


Wakati wa ujauzito kuna mabadiliko ya homoni yanayoweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kupata maambukizi ya fangasi ukeni, tafiti zinaonyesha kuwa maambukizi ukeni hutokea sana kipindi hiki kutokana na mabadiliko ya utindikali wa uke unaosababishwa na mabadiliko ya homoni.


Dalili za fangasi ukeni kwenye ujauzito


Dalili za fangasi ukeni wakati wa ujauzito ni;


Ongezeko la ute unaotoka ukeni unaoambatana na sifa zifuatazo;


  • Kuwa mweupe kama pamba au kama maziwa mgando

  • Ute usio na harufu mara nyingi, hata hivyo unapokuwa na harufu hunuka kama mkate

  • Kuwashwa maeneo yanayozunguka tundu la na mashavu ya uke


Vihatarishi


Mambo yafuatayo yanaongeza hatari ya kupata fangasi ukeni kwenye ujauzito;


  • Matumizi ya dawa za uzazi wa mpango

  • Matumizi ya antibayotiki au dawa jamii ya steroid

  • Kuwa na kiwango cha juu cha sukari kama kwa wagonjwa wa kisukari

  • Kushiriki ngono

  • Kujisafisha na kemikali au sabuni ukeni

  • Kutumia marashi ya kuweka ukeni

  • Damu ukeni au kuwa na shahawa kutokana na kutojisafisha


Magonjwa mengine yanayosababisha uchafu ukeni kwenye ujauzito


Magonjwa mengine yanayoweza kuleta dalili kama hizi ni;



Vipimo na utambuzi


Mara nyingi daktari atatambua kwa kutumia historia ya tatizo lako baada ya kukuulzia maswali, endapo atataka kutofautisha na magonjwa mengine au kuthibitisha, ataagiza vipimo vifuatavyo kufanyika;


  • Kipimo cha culture ya majimaji kutoka ukeni

  • Kipimo cha syphilis


Ni dawa gani unapaswa kutumia wakati wa ujauzito kutibu fangasi ukeni?


Si dawa zaote unapaswa kutumia wakati wa ujauzito kwa matibabu ya fangasi ukeni. Dawa nyingi zinazotumika ni zile za kuweka ukeni au kupaka. Dawa za kumeza za fangasi hazishauriwi kutumika, wasiliana na daktari wako kwa ushauri zaidi wa dawa gani inakufaa. Unaweza kusoma 'dawa za kutibu fangasi ukeni' kwenye makala zingine ndani ya tovuti hii.


Wakati gani uwasiliane na daktari?


Unapaswa kuhofu kuwa una maambukizi ukeni au tatizo la kufanyiwa uchungnzi wa haraka endapo uchafu au ute wenye sifa zifuatazo unatoka ukeni;


  • Ute wenye rangi ya njano

  • Ute wa kijani

  • Ute wa kijivu

  • Ute wenye harufu kali au ya kuoza

  • Ute mweupe mzito kama maziwa mgando

  • Ute wenye rangi nyekundu ( damu mbichi)

  • Ute unaoambatana na muwasho, wekundu au kuvimba kwa mashavu ya uke

  • Ute unaoambatana na harufu kali au kama ya samaki

  • Ute unaoambatana na maumivu ya tumbo la chini au wakati wa kukojoa


Ukitokwa na ute au uchafu wenye rangi na sifa zilizotajwa hapo juu kwenye ujauzito wasiliana na daktari wako kwa uchuguzi na tiba.

Kinga ya maambukizi ya fangasi ukeni kwenye ujauzito


Ili kujikinga na maambukizi ya fangasi kwenye ujauzito, fanya mambo yafuatayo


  • Vaa nguo zisiyobana na inayoruhusu hewa kuingia mwilini

  • Tumia nguo za ndani zenye pamba

  • Kausha maeneo ya uke baada ya kuoga au kufanya mazoezi

  • Kula vyakula vya maziwa mgando na ingine vilivyochachushwa ili kufanya bakteria walinzi waongezeke ukeni

  • Usitumie manukato ya kuweka ukeni

  • Jisafishe uke kutoka mbele kwenda nyuma badala ya nyuma kwenda mbele kuepuka kutia uchafu au majimaji ya njia ya haja kubwa ukeni


Sehemu gani nyingine unaweza kupata taarifa zaidi?


Pata taarifa zaidi kuhusu ute unaotoka ukeni, rangi ya kawaida na isiyo ya kawaida na maana yake kiafya kwa kubofya linki inayofuata.


1. https://www.ulyclinic.com/post/rangi-ya-majimaji-ukeni-na-maana-zake-kiafya-uly-clinic


Majina mengine ya tatizo la fangasi ukeni kwenye ujauzito


Baadhi ya watu hufahamu tatizo hili kama;


  • Kutokwa na maziwa ukeni wakati wa ujauzito

  • Uchafu mweupe mzito ukeni wakati wa ujauzito

  • Kuwashwa ukeni wakati wa ujauzito

  • Kutokwa na maji yasiyo ya kawaida ukeni wakati wa ujauzito

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba kabla ya kuchukua hatua yoyote ya kitiba baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kubofya 'Pata Tiba,  au ''mawasiliano yetu' chini ya tovuti hii

Imeboreshwa,

13 Julai 2023 19:02:51

Rejea za mada hii:

bottom of page