Mwandishi:
Mhhariri
ULY CLINIC
Dkt. Lugonda S, MD
Jumatatu, 8 Novemba 2021
Kuvimba tonsil
Tonsil ni mkusanyiko wa chembe nyeupe za damu zinazopambana na magonjwa katika kinywa zilizo karibu na koo. Mbali na kuwa na tezi za tonsil, kinywa huwa pia na tezi za adenoid ambazo ni mkusanyiko wa tishu zinazozalisha chembe nyeupe za damu katika kinywa. Tonsil na adenoid hufanya kazi za ulinzi wa kinywa dhidi ya vimelea wanaotaka kuingia kupitia mdomo, pua au masikio.
Kazi za tezi za tonsil na adenoid
Kazi za tezi hzi ni kutoa kemikali ambazo hupambana na maradhi kinywani. Tezi hizi zinazokaa pambe zote
za kinywa hufanya kazi ya kupambana na maradhi yanayoingia kupitia kinywa , mara nyingi tezi hizi huanza kufanya kazi kwa kiasi kikubwa binadamu anapofikia umri wa miaka 4 hadi 10 na baadae hupunguza kazi baada ya kubarehe. Hii ndio maana ugonjwa wa tonsil husumbua sana watoto wadogo ukilinganisha watu wakubwa. Ingawa tafiti zinaonyesha kuwa kutolewa kwa tezi kinywa huwa haisababishi kupugua kwa kinga ya mwili dhidi ya maradhi.
Matokeo ya maambukizi ya mara ya kwanza
Mara nyingi maambukizi ya awali ya tonsil husababishwa na virus, maambukizi ya bakteria haswa aina ya streptococcus.
Maambukizi ya fungusi katika kinywa huweza kutokea kwa watu walio na kinga ya mwili ya chini, au watoto na watu wakubwa waliotibiwa na kwa matibabu ya madawa ya kupambana na bakteria.
Maambukizi sugu
Maambukizi sugu ya tonsil na tezi koo husababishwa na vimelea aina kadhaa ambao ni bakteria, bakteria wanaoishi bila oksigen na wale wanaoishi kwenye oksigen.
Dalili za kuvimba tonses
Dalili za ugonjwa wa tonsils
Kuziba kwa njia ya hewa
Mtu atapata dalili kama, kushindwa kupumua na kupumua kwa shida-kwa watoto na dalili zingine kama
kushindwa kumeza,
koo kuwa kavu,
mwili kuchoka,
homa na mwili kutetemeka,
Masikio kuuma,
Kichwa kuuma,
Misuli kuuma,
Kuvimba kwa mitoki ya shingo.,
Tezi kuwa nyekundu na kuvimba,
Kutokwa na uchafu kinywani na maumivu.
Kuvimba kwa tezi ya upande mmoja wa kinywa huweza humaanisha saratani ya chembe za mitoki
Dalili za usugu
Maambukizi sugu ya tezi kinywa husababisha dalili kama;
Harufu mbaya mdomoni,
Koo kuwa chungu,
Hisia za kitu kigeni au kizito kwenye koo,
Historia ya kutema vitu vitu vichafu kutoka kooni.
Mtoto akiangaliwa kinywani tezi huonekana kuwa zimevimba (Angalia picha)
Matibabu
Matibabu yapo ya aina mbili- matibabu dawa na matibabu ya upasuaji
Matibabu dawa ya maambukizi sugu ya tezi shingo huwa hayasikii dawa za penicillin kwa sababu husababishwa na mchanganyiko wa vimelea.
Pia kwa watoto wenye maambukizi sugu wanaweza kuwa na mabaki/uchafu kwenye tezi na hivyo matumizi ya pamba kuondoa uchafu huo ama maji yanaweza kutumika.
Matibabu ya upasuaji hutumika na hutibu tatizo sugu la maambukizi ya tezi koo na hutibu kwa asilimia kubwa na huzuia maambukizi yanajirudia rudia.
Soma makala nyingine kuhusu mawe kwenye tezi ya tonsil au tonsilithi kwa kubonyeza hapa
​