top of page

Magonjwa na saratani mbalimbali

Sehemu hii utasoma kuhusu hali na magonjwa mbalimbali

Uvimbe maji kwenye Ovari (Sisti)

Uvimbe maji kwenye Ovari (Sisti)

Ni uvimbe unaoweza kuwa na majimaji au tishu na huwa si saratani. Sisti ndogo, rahisi, yenye majimaji pekee, isiyo na dalili na yenye muonekano wa kawaida kwenye ultrasound mara nyingi hufuatiliwa tu na huweza kutoweka yenyewe. Sisti kubwa, inayoendelea kukua au kuwepo, yenye muonekano changamano/sehemu ngumu, inayosababisha dalili kubwa au yenye viashiria vya saratani inaweza kuhitaji uchunguzi zaidi na wakati mwingine upasuaji kulingana na tathmini ya daktari.

Folikulaitisi: Uvimbekinga wa vinyeleo

Folikulaitisi: Uvimbekinga wa vinyeleo

Ni kuvimba kwa vinyweleo ambako kunaweza kusababisha vipele vidogo, kuwasha, maumivu au usaha, na huweza kuchochewa na bakteria, fangasi, jasho, msuguano au kunyoa. Kutambua chanzo ni muhimu kwa matibabu sahihi, hasa ikiwa vipele vinajirudia, vinaacha makovu au haviponi baada ya hatua za kawaida za kutunza ngozi.

Furunkulosisi: Majipu yanayojirudia

Furunkulosisi: Majipu yanayojirudia

Mara nyingi husababishwa na maambukizi ya bakteria, hujidhihirisha kwa majipu yenye maumivu, uvimbe, joto na usaha, na yanaweza kuacha makovu au mabaka meusi, kahawia au zambarau baada ya kupona. Homa, maambukizi yanayoenea haraka, maumivu makali, majipu makubwa au yanayojirudia mara kwa mara ni dalili za hatari zinazohitaji uchunguzi wa mtaalamu wa afya.

Keratosisi pilarisi

Keratosisi pilarisi

Ni hali ya kawaida ya ngozi inayosababisha vijipele vidogo na ukavu, hasa kwenye mikono, mapaja, makalio na wakati mwingine usoni. Si ugonjwa hatari wala wa kuambukiza, lakini inaweza kudumu kwa muda na kudhibitiwa kwa utunzaji sahihi wa ngozi na matibabu yanayofaa.

bottom of page