Sehemu hii utasoma kuhusu hali na magonjwa mbalimbali
Kichaa cha mbwa: Sababu, Dalili, Vipimo na Matibabu
Kichaa cha mbwa ni ugonjwa hatari wa virusi unaoathiri mfumo wa neva na karibu kila mara husababisha kifo dalili zikishaanza. Kinga ya mapema baada ya kung’atwa au kukwaruzwa na mnyama mwenye maambukizi huokoa maisha.
Pangusa: Visababishi, Dalili, Matibabu na Namna ya Kujikinga
Pangusa ni ugonjwa wa zinaa unaosababisha vidonda laini vinavyouma kwenye sehemu za siri pamoja na uvimbe wa tezi limfu kwenye kinena. Husababishwa na Haemophilus ducreyi na hutibika kwa dawa za antibayotiki.
Uvimbe wa Batholini: Sababu, Dalili, Matibabu na Namna ya Kujikinga
Uvimbe wa Batholini ni hali inayotokea kutokana na kuziba kwa tezi karibu na mlango wa uke, na unaweza kuwa na maumivu au bila. Ingawa si hatari kwa maisha, huhitaji usafi na tiba sahihi ili kupona na kuepuka maambukizi.
Homa ya ini ni ugonjwa wa kuvimba kwa ini unaosababishwa na virusi, ambao unaweza kuwa wa muda mfupi au wa kudumu. Ikiwa haitatibiwa mapema, huweza kusababisha madhara makubwa kama sirosisi, saratani ya ini, au kifo.