Mwandishi:
Mhhariri
ULY CLINIC
Dkt. Mangwella S, MD
Jumanne, 6 Aprili 2021

Maumivu ya korodani kutokana na Epididymitis
Epididymitis ni neno tiba lenye maana ya uvimbe wa mirija ya epididymis kutokana na mwitikio wa chembe hai za mwili dhidi ya maambukizi au kitu kigeni kwenye mirija hiyo. Mirija ya epidydimis huwa ipo nyuma ya korodani ambayo huwa na sura ya kujizungusha kama koili. Kazi za mirija hii ni kutunza shahawa.
Ni nini husababisha Epididymitis
Kisababishi kukuu kwa vijana wenye umwi chini ya miaka 35 huwa ni maambukizi ya magonjwa ya zinaa ambayo ni
Kisonono
Chlamydia
Hata hivyo maambukizi ya UTI (Escherichia coli) yanaweza kusambaa kutoka kwenye tezi dume kuja kwenye mirija hii na kuleta maambukizi
Visababishi vingine vya epidydymitis kwa vijana wa umri wa miaka 35 au zaidi
Maambukizi kutoka kwenye tezi dume
Mkojo kuingia kwenye mirija ya epidydimis
Kupata jeraha kwenye korodani
Maambukizi ya TB kwenye korodani
Maambukizi ya virusi na fangasi kwa wagonjwa wenye kinga za chini na wenye UKIMWI/Kisukari
Sababu zisizojulikana
Dalili za Epididymitis
Dalili za epididymitis huwa kati ya zifuatazo;
Kuvimba na kubadilika rangi kwa pumbu
Maumivu ya korodani zikishikwa, mara nyingi huwa upande mmoja tu na maumivu huanza taratibu
Maumivu wakati wa kukojoa au kupata hamu ya kukojoa ghafla
Kutokwa na uchafu kwenye uume
Maumivu ya tumbo la chini au kwenye nyonga
Kutokwa na damu kwenye shahawa
Kwa nadra sana unaweza pata homa
Kumbuka
Dalili hutegemea hatua ya ugonjwa, hivyo unaweza kuwa na dalili mbili au zaidi ili kusemekana kuwa una maambukizi haya.
Vihatarishi vya ugonjwa wa epidydymitis
Vitu au mambo yafuatayo yanakuweka kwenye hatari ya kupata maambukizi haya
Kuwa na wapenzi wengi
Kutotumia kodomu wakati wa kufanya ngono
Kuwa na historia ya kuumwa magonjwa ya zinaa
Historia ya maambukizi kwenye tezi dume(prostatitis) au UTI
Kufanyiwa upasuaji kwenye njia ya mkojo
Kuwekewa mrija wa mkojo kwenye uume
Kutotahiliwa
Kukua kwa tezi dume
Vipimo vya kutambua ugonjwa wa epidydymitis
Mara utakapofika hospitali utaulizwa maswali mbalimbali yanayolega kufahamu visababishi kama vilivyoandikwa hapo juu kisha daktari ataagiza vipimo kulingana na nini ameona ni shida. Vipimo huhusisha;
Kuchukuliwa ute kutoka ndani ya uume wako kwa ajili ya kipimo cha magonjwa ya zinaa
Kipimo cha urine culture
Kipimo cha damu kuangalia kama kuna shida yoyote
Kipimo cha mkojo kuangalia kama kuna shida yoyote kwenye mkojo
Kipimo cha ultrasound kuangalia hali ya mirija ya epidydimis pamoja na korodani na kutofautisha tatizo hili na magonjwa mengine kama kujisokota kwa moroja ya korodani n.k
Madhara ya ugonjwa wa epidydymitis
Madhara yafuatayo yanawez akutokea endapo matibabu hayajafanyika kwa wakati
Kujaa kwa usaha ndani ya pumbu
Kupata ugonjwa wa epidydimo-orchitis
Ugumba
Wakati gani mgonjwa wa epididymitis amwone daktari?
Ni vema mara baada ya kuanza kuhisi maumivu ya korodani kumwona daktari wako haraka ili kufanyiwa uchunguzi na tiba kabla ya tatizo kuwa kubwa. Kumbuka korodani ni kitu cha muhimu sana.
Matibabu ya ugonjwa wa epididymitis
Matibabu husisha;
Dawa
Upasuaji
Dawa
Dawa za kutibu magojwa ya zinaa au UTI, mpenzi wako pia atahitaji matibabu ili kuondoa kihatarishi cha kupata maambukizi kutoka kwake kwa mara nyingine. Utapswa kumaliza dozi uliyopewa hatakama zitapotea kabla ya kumaliza dozi
Endapo una maumivu, tumia dawa za kuondoa maumivu kama parasetamo.
Upasuaji
Hufanyika kwa watu wenye usaha kwenye korodani, upasuaji hufanyika kuondoa usaha kwenye korodani na kufanya zipone haraka. Baadhi ya wakati itahitajika kuondoa sehemu ya mirija ya epidydimis.
Matibabu ya upasuaji wa kuondoa mrija(mirija) ya epididymis huweza hitajika fanyika kwa wagonjwa ambao wanapata maambukizi kujirudia kwenye tezi dume(prostatitis) au mrija wa urethra (urethritis)
Namna ya kujikinga na ugonjwa wa epididymitis
Fanya mambo yafuatayo ili kujikinga na tatizo hili;
Tumia kondomu unaposhiriki ngono
Pata matibabu sahihi ya UTI ya kujirudia na kwa wakati
Matibabu ya nyumbani ya ugonjwa wa epididymitis
Endapo una tatizo hili fanya mambo yafuatayo kupunguza dalili
Pumzika kwa kulala kitandani huku korodani zikiwa juu
Tumia barafu kukanda eneo lenye maumivu ya korodani jinsi unavyoweza
Usinyanyue mizigo mizito
Usishiriki mapenzi mpaka upone kabisa