top of page

Mwandishi:

Mhhariri

ULY CLINIC

Dkt. Mangwella S, MD

Ijumaa, 5 Novemba 2021

Vidonda kwenye ulimi

Vidonda kwenye ulimi

Vidonda kwenye ulimi huweza kuonekana Kama vijishimo vidogo vyenye rangi nyeupe au njano kwenye ulimi au kwenye fizi chini kidogo ya meno.


Visababishi


Vidonda hivi huitwa canker, huwa haviambukizwi na mara nyingi husabaishwa na vitu tunavyotumia kila siku kama kemikali kwenye dawa za miswaki, dawa za kuosha mdomo, mzio wa chakula, au upungufu wa vitamin aina fulani mwilini. Wakati mwingine hakuna kisababishi kinachojulikana kusababisha vidonda hivi.


Visababishi vingine

Visababishi vingine vya maumivu ya ulimi huwa pamoja na;


  • Saratani

  • Upungufu wa damu

  • Maambukizi ya virusi vya Herpes

  • Kuvaa vidani kwenye ulimi

  • Matatizo ya mishipa ya fahamu

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba kabla ya kuchukua hatua yoyote ya kitiba baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kubofya 'Pata Tiba,  au ''mawasiliano yetu' chini ya tovuti hii

Imeboreshwa,

13 Julai 2023 19:03:22

Rejea za mada hii:

bottom of page