top of page

Majibu ya maswali mbalimbali

Njia za kuzuia kutungwa kwa mimba, njia za kuzuia mimba

Njia za kuzuia mimba kutungwa

Njia za kuzuia mimba husaidia kuzuia urutubishaji au kuzuia yai lililorutubishwa kujishikiza kwenye mfuko wa mimba, hivyo kuzuia ujauzito kutokea. Kuna njia za muda mfupi, muda mrefu, za dharura, pamoja na za kudumu kila moja ikiwa na ufanisi, matumizi, na faida tofauti kutegemea mahitaji ya mwanamke au mwanaume.

Tatizo la kukosa usingizi

Kukosa usingizi

Kukosa usingizi (Insomnia) ni hali ya kushindwa kuanza kulala, kudumu usingizini au kuamka mapema licha ya kuwa na mazingira mazuri ya kulala. Hali hii hupunguza ufanisi wa mchana na huathiri afya ya mwili, akili na ubora wa maisha.

Kukokotoa siku ya uovuleshaji, uhesabuji wa siku ya uovuleshaji, ukokotoaji wa siku ya kushika mimba

Kukokotoa siku ya uovuleshaji

Tarehe ya uovuleshaji huhesabiwa kuanzia siku ya kwanza ya hedhi kwa sababu hiyo ndiyo siku ya kwanza ya mzunguko mpya wa homoni na kukomaa kwa yai huanza hapo. Kuisha kwa hedhi hakuathiri uovuleshaji, hivyo tarehe ya uovuleshaji hupatikana kwa mahesabu ya urefu wa mzunguko wa siku 14.

Nywele kukua ndani sehemu za siri: Sababu, Dalili na Tiba

Nywele kukua ndani sehemu za siri: Sababu, Dalili na Tiba

Nywele kukua ndani sehemu za siri husababisha uvimbe, wekundu na maumivu kutokana na nywele kujikunja au kushindwa kutoka juu ya ngozi, mara nyingi baada ya kunyoa au msuguano. Tatizo hutibika kwa compres ya maji ya uvuguvugu, kusafisha ngozi, exfoliation, na wakati mwingine dawa za hospitali iwapo kuna maambukizi.

Mwasho wa Ngozi: Sababu, Uchunguzi na Matibabu

Mwasho wa Ngozi: Sababu, Uchunguzi na Matibabu

Mwasho wa ngozi ni hisia ya kero inayosababisha kujikuna, ikihusiana na visababishi mbalimbali ikiwemo ngozi kavu, magonjwa ya ndani, aleji, madawa, na ujauzito. Matibabu yanahusisha kudhibiti mwasho, kutibu chanzo cha msingi, na kuchukua hatua za kinga nyumbani ili kuzuia kujeruhiwa kwa ngozi na maambukizi.

Magonjwa yanayoonekana kwa kupima damu

Magonjwa yanayoonekana kwa kupima damu

Kupima damu husaidia kubaini magonjwa mengi muhimu kama anemia, kisukari, maambukizi, magonjwa ya figo, ini, tezi na matatizo ya moyo. Ni kipimo rahisi lakini chenye taarifa pana kinachowezesha utambuzi wa mapema na kufuatilia maendeleo ya matibabu.

Kipimo cha mkojo kuonyesha uwepo wa damu (Hematuria): Maana, na Hatua za kuchukua

Kipimo cha mkojo kuonyesha uwepo wa damu (Hematuria): Maana, na Hatua za kuchukua

Kipimo cha mkojo kuonyesha damu (hematuria) kinaashiria hali mbalimbali kama maambukizi, mawe, magonjwa ya figo, majeraha au saratani, na hutegemea uchunguzi wa ziada kubaini chanzo. Matibabu hutolewa kulingana na kisababishi, kuanzia antibayotiki, kudhibiti shinikizo la damu, kuvunja mawe, hadi upasuaji kwa saratani au majeraha makubwa.

Hedhi wakati wa matumizi ya uzazi wa mpango: Sifa na wakati wa kumwona daktari

Hedhi wakati wa Uzazi wa mpango: Sifa na lini utafute msaada

Hedhi inaweza kubadilika wakati wa kutumia njia za uzazi wa mpango kutokana na athari za vichochezi kwenye mzunguko wa homoni. Mabadiliko haya huwa ya muda na mara nyingi hurudi kuwa ya kawaida baada ya kuacha kutumia njia husika.

Kutokwa ute mweupe kama krimu ukeni wakati wa tendo la ndoa

Kutokwa ute mweupe kama krimu ukeni wakati wa tendo la ndoa

Kutokwa na kremu nyeupe ukeni wakati wa tendo mara nyingi ni hali ya kawaida inayotokana na msisimko wa kimapenzi na mabadiliko ya ute wa uke.
Hata hivyo, mabadiliko ya harufu, rangi, wingi au maumivu yanaweza kuashiria fangasi, BV au STIs, hivyo vipimo na matibabu mapema ni muhimu.

Je, inawezekana kuambukizwa Virusi vya UKIMWI au magonjwa mengine ukikatwa na bati kama mtu mwingine alikatwa pia?

Je, inawezekana kuambukizwa Virusi vya UKIMWI au magonjwa mengine ukikatwa na bati kama mtu mwingine alikatwa pia?

Kukatwa na bati kunaweza kusababisha maambukizi, lakini hatari ya kupata VVU ni ndogo sana isipokuwa damu mpya ya muathirika iingie moja kwa moja kwenye jeraha lako. Hatari kubwa zaidi ni tetanasi na hepatitis, hivyo ni muhimu kusafisha jeraha, kupata chanjo ya tetanasi, na kumwona daktari kwa tathmini.

Kusimama kwa hedhi, kutoingia hedhi

Kusimama kwa hedhi

Kutoona hedhi (amenorea) ni hali ambapo mwanamke hukosa damu ya hedhi kutokana na mabadiliko ya homoni, maisha, au matatizo ya kimaumbile. Uchunguzi wa kitabibu na matibabu sahihi husaidia kurejesha mzunguko wa hedhi na kulinda afya ya uzazi.

Kubadilika badilika kwa tarehe ya kuingia Hedhi: Sababu, Athari, na Ushauri kwa Wagonjwa

Kubadilika badilika kwa tarehe ya kuingia Hedhi: Sababu, Athari, na Ushauri kwa Wagonjwa

Kubadilika kwa tarehe ya kuingia hedhi ni jambo la kawaida linaloweza kusababishwa na mabadiliko ya homoni, msongo wa mawazo au matatizo ya kiafya. Ufuatiliaji wa mzunguko, vipimo sahihi na matibabu kulingana na chanzo husaidia kurejesha mzunguko wa hedhi katika hali ya kawaida.

bottom of page