top of page

Mwandishi:

ULY CLINIC

Mhariri:

Dkt. Benjamin L, MD

14 Novemba 2021 08:22:42

Je, ni madhara gani ya gono kwa mjamzito?

Madhara ya gono kwa mjamzito

Gono ni jina linalotumika na watu wengi lililotokana na ugonjwa gonorrheal na huwa na maana pia ya kisonono. Ugonjwa huu husabaishwa na bakteria mwenye jina la Neisseria gonorrhea ambaye huenezwa kwa kujamiana na mtu mwenye maambukizi bila kutumia kinga.


Madhara kwa mama mjamzito


Yapo madhara kadha wa kadhayanayoweza kutokea wakati wa ujauzito kama mama mjamzito asipopata matibabu ya gono ambayo ni;


  • Mtoto kuzaliwa akiwa na upofu

  • Kuharibika kwa mimba

  • Kujifungua njiti

  • Kujifungua mtoto mwenye uzito mdogo

  • Kupasuka kwa chupa ya uzazi kabla ya wakati

  • Maambukizi kwenye chupa ya uzazi


Kusoma zaidi kuhusu gono, vihatarishi na madhara kwa ujumla ingia kwenye makala ya gono.

ULY CLINIC inakushauri uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba kabla ya kuchukua hatua yoyote ile baada ya kusoma majibu haya.

Kupata ushauri zaidi au tiba kutoka kwa daktari wa ULY CLINIC bofya hapa au tumia linki ya Pata tiba

Imeboreshwa,

14 Novemba 2021 19:18:49

Rejea za mada hii

  1. CDC. S.T.I in pregnancy. https://www.cdc.gov/std/pregnancy/stdfact-pregnancy-detailed.htm. Imechukuliwa 14.11.2021

bottom of page