top of page

Mwandishi:

ULY CLINIC

Mhariri:

Dkt. Benjamin L, MD

16 Julai 2025, 14:37:48

Koo kuwaka moto mpaka masikioni: Sababu, Uchunguzi na Matibabu?

Koo kuwaka moto mpaka masikioni: Sababu, Uchunguzi na Matibabu?

Swali la msingi

"Habari daktari, nahisi koo langu linawaka moto sana hadi maumivu yanaenda hadi kwenye masikio. Kila nikimeza naona uchungu mkali. Hadi nahisi kuchanganyikiwa. Je, hili ni tatizo kubwa? Linahitaji vipimo gani? Naweza kupata dawa gani?"


Majibu

Maumivu ya koo ni moja ya sababu kuu zinazowapeleka watu hospitali, hasa yanapokuwa makali na kuenea hadi masikioni. Wakati mwingine, mtu huhisi kana kwamba koo linawaka moto, huwezi kumeza, na hata maumivu huenda upande mmoja wa sikio. Hali hii inaweza kuambatana na homa, kizunguzungu au hata kuchoka sana.


Makala hii inalenga kutoa elimu sahihi kuhusu visababishi vinavyoweza kuleta hisia hii kali ya "koo kuwaka moto hadi masikioni," vipimo muhimu, namna ya kupata tiba, na wakati wa kumwona daktari. Kusoma makala hii kutakusaidia kuelewa chanzo cha tatizo lako na hatua salama za kuchukua.


Dalili

Dalili za kawaida zinazoweza kuambatana na Koo linalowaka moto ni pamoja na;

  • Maumivu makali ya koo

  • Kumeza chakula au mate kwa shida

  • Kichefuchefu au kutoona hamu ya kula

  • Maumivu ya masikio (hasa upande mmoja au yote)

  • Kichwa kuuma na mwili kulegea

  • Kuvimba kwa tezi za shingo

  • Homa kali au kutetemeka


Visababishi vya koo kuwaka moto

Baadhi ya visababishi vikuu ni pamoja na;


1. Tonsillitis (Uvuvimbe wa tezi tonses)
  • Huambatana na koo kuwaka, maumivu hadi kwenye masikio

  • Mara nyingi husababishwa na virusi au bakteria

  • Mdomo unaweza kuwa na harufu, mate mengi au mawe madogo meupe kwenye tonsils


2. Uvuvimbe wa nyuma ya koo
  • Koo linakuwa jekundu, lenye maumivu makali

  • Husababisha hisia ya kuwaka moto hadi kwenye sikio

  • Huambatana na kikohozi au mafua

  • Husababishwa na maambukizi ya virusi au bakteria kwenye koo au kuunguzwa na tindikali ya tumboni


3. Maambukizi ya sikio la kati
  • Maumivu ya koo yanayoambatana na presha au maumivu ya ndani ya sikio

  • Huenda na kikohozi, baridi au mafua yaliyodumu


4. Kucheua tindikali
  • Hutokana na asidi ya tumbo kupanda kooni

  • Koo kuwaka moto hasa asubuhi au baada ya kula

  • Maumivu huenda hadi masikioni, hususani ukilala bila mlo kushuka vizuri


5. Uvuvimbe wa tezi ya Adenoid au Sainaz
  • Hali ya uvimbe au maambukizi nyuma ya pua (nasopharynx) hupelekea koo kuwaka hadi masikio

  • Huziba pua, kuleta harufu mbaya mdomoni, na presha ya sikio


Vipimo na uchunguzi

Vipimo vinavyoweza kufanyika (Kulingana na Dalili) ni pamoja na;

Jina la Kipimo

Maelezo

Kipimo cha ute kwenye koo

Kupima bakteria (kama Streptococcus pyogenes)

Kipimo cha hesabu kamili ya damu

Kuangalia wingi wa chembe nyeupe (dalili za maambukizi)

Uchunguzi wa koo na sikio

Kuangalia sikio kwa kifaa maalumu kutathmini kama kuna maambukizi

Uchunguzi wa pua, koo na umio kwa kamera

Daktari kutazama nyuma ya pua na koo kwa kifaa maalumu


Matibabu

Matibabu hunategemea Kisababishi kama yalivyorodheshwa katika jedwali hapo chini;

Sababu ya Koo Kuwaka moto

Dawa zinazotumika

Virusi (Homa ya baridi, homa ya mafua)

Paracetamol, maji mengi, kupumzika

Bakteria (Maambukizi kwenye tesi tonses kutokana na bakteria)

Antibayotiki kama Amoxicillin au Azithromycin (kwa ushauri wa daktari)

Kucheu tindikali

Dawa za kupunguza uzalishaji wa asidi tumboni(Omeprazole, Ranitidine)

Maambukizi kwenye sikio la kati

Antibiotics + painkillers + ear drops

Maambukizi ya sinus au pua

Dawa za kukausha kamasi, antibayotiki, mvuke moto


Huduma za nyumbani za koo kuwaka moto

  • Kunywa maji ya uvuguvugu mara kwa mara

  • Tumia tangawizi, asali na ndimu katika chai

  • Epuka vinywaji vya baridi au vyenye cafeini

  • Tumia mvuke wa maji moto (steam inhalation)

  • Pumzika na usijibebeshe shughuli nyingi


Wakati gani wa kumwona daktari haraka?

  • Ikiwa koo linawaka hadi huwezi kumeza kabisa

  • Kikohozi cha damu au mate ya njano kijani

  • Homa kali inayozidi siku 3

  • Maumivu ya sikio makali au kutokwa na usaha

  • Kizunguzungu, kupumua kwa shida, au tezi kuvimba shingoni


Hitimisho

Koo kuwaka moto hadi masikioni ni dalili ya maambukizi, uvimbe au matatizo ya koo, pua au sikio. Chanzo sahihi hupatikana kwa vipimo sahihi. Matibabu yanatolewa kulingana na kisababishi, na hali nyingi huweza kupona kabisa kwa tiba stahiki au hata huduma za nyumbani.

ULY CLINIC inakushauri uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba kabla ya kuchukua hatua yoyote ile baada ya kusoma majibu haya.

Kupata ushauri zaidi au tiba kutoka kwa daktari wa ULY CLINIC bofya hapa au tumia linki ya Pata tiba

Imeboreshwa,

16 Julai 2025, 14:37:48

Rejea za mada hii

  1. Brook I. Management of Acute Pharyngotonsillitis in Children and Adults. J Fam Pract. 2019;68(4):207–212.

  2. Shulman ST, et al. Clinical Practice Guideline for the Diagnosis and Management of Group A Streptococcal Pharyngitis. Clin Infect Dis. 2012;55(10):1279–1282.

  3. National Institutes of Health (NIH). Otitis Media in Children and Adults. Updated 2023.

  4. Johns MM, et al. GERD-related laryngitis and sore throat. Otolaryngol Clin North Am. 2013;46(6):1071–1082.

  5. UpToDate. Evaluation of sore throat in children and adults. Wolters Kluwer Health; 2024.

bottom of page