Mwandishi:
ULY CLINIC
Mhariri:
Dkt. Glory M, MD
21 Machi 2025, 05:42:50

Nini husababisha kutokwa na damu katikati ya mzunguko wa hedhi?
Kutokwa na damu katikati ya mzunguko wa hedhi ni hali ambapo mwanamke hupata damu kutoka ukeni nje ya kipindi chake cha kawaida cha hedhi. Hali hii inaweza kusababishwa na mabadiliko ya homoni, maambukizi, au magonjwa makubwa kama saratani ya kizazi.
Makala hii imezungumzia kuhusu visababishi, dalili, uchunguzi, na Matibabu ya tatizo la tatizo la kutokwa na damu katikati ya mzunguko wa Hedhi.
Kumbuka: Kutokwa na damu katikati ya mzunguko wa hedhi katika makala hii imemaanisha kutokwa na damu kipindi chochote kile kabla ya tarehe ya hedhi inayofuata kuwadia.
Visababishi vya kutokwa na damu katikati ya Hedhi
Kisababishi | Dalili | Uchunguzi | Matibabu |
Mabadiliko ya Homoni | Mizunguko ya hedhi isiyo ya kawaida, matone ya damu kidogo kati ya hedhi | Vipimo vya homoni (FSH, LH, estrogen, progesterone), ultrasound | Vidonge vya kupanga uzazi, tiba ya homoni |
Kutokwa na Damu Wakati wa Ovulation | Matone ya damu katikati ya mzunguko wa hedhi, maumivu ya wastani ya upande yai lilipotolewa | Historia ya hedhi, kufuatilia ovulation | Haihitaji matibabu maalumu |
Ugonjwa wa Ovari yenye vifuko maji vingi (PCOS) | Hedhi isiyo ya kawaida, chunusi, unene, kuwa nanywele nyingi mwilini | Ultrasound ya nyonga, vipimo vya homoni | Mabadiliko ya mtindo wa maisha, dawa za homoni (OCPs, metformin) |
Uvimbe kwenye Kizazi (Fibroid) | Hedhi nzito, maumivu ya nyonga, kukojoa mara kwa mara | Uchunguzi wa nyonga, ultrasound, MRI | Dawa za kupunguza uvimbe, upasuaji (Kuondoa uvimbe au kizazi) |
Vinundu ndani ya mji wa mimba (Polyps) | Kutokwa na damu kati ya hedhi, hedhi nzito | Ultrasound, hysteroscopy | Upasuaji wa kuondoa vinundu |
Endometriosis | Maumivu makali ya hedhi, maumivu ya nyonga, utasa | Laparoscopy, ultrasound | Dawa za kupunguza maumivu, tiba ya homoni, upasuaji |
Maambukizi kwenye via vya uzazi (PID) | Maumivu ya nyonga, uchafu usio wa kawaida, homa, maumivu wakati wa ngono | Uchunguzi wa nyonga, vipimo vya maambukizi kwenye ute ukeni na Ultrosound | Antibiotiki, dawa za kupunguza maumivu |
Saratani ya shingo ya kizazi au saratani ya kizazi | Kutokwa na damu baada ya hedhi, hedhi nzito, maumivu ya nyonga | Pap smear, biopsy, MRI | Upasuaji, tiba ya mionzi, kemotherapi |
Magonjwa ya Zinaa (Klamidia, Kaswende, Kisonono, n.k.) | Uchafu ukeni wenye harufu mbaya, maumivu ya nyonga, damu baada ya tendo la ndoa | Vipimo vya magonjwa ya zinaa (PCR, culture) | Antibiotiki |
Matumizi ya dawa za kuzuia mimba (IUD, Vidonge, sindano za depo-provera) | Kutokwa na damu isiyo ya kawaida, mzunguko wa hedhi kubadilika | Historia ya uzazi wa mpango, ultrasound kurekebisha mkao wa IUD | Kubadilisha njia ya uzazi wa mpango |
Msongo wa mawazo na mtindo wa maisha | Hedhi isiyo ya kawaida, mabadiliko ya mhemko | Tathmini ya maisha na historia ya mgonjwa | Kudhibiti msongo wa mawazo, kula vizuri, kufanya mazoezi |
Matumizi ya dawa (za kuyeyusha damu, Tiba ya Homoni, korticosteroids) | Kutokwa na damu isiyoeleweka | Historia ya matumizi ya dawa, vipimo vya damu | Kubadilisha au kurekebisha dawa |
Uchunguzi wa Kutokwa na Damu Kati ya Hedhi
Ili kubaini chanzo cha tatizo, daktari anaweza kufanya mambo na vipimo vifuatavyo:
i) Historia ya Matibabu na uchunguzi wa kimwili
Historia ya mzunguko wa hedhi
Historia ya matumizi ya njia za uzazi wa mpango
Dalili zinazofuatana na kutokwa damu (uchungu, homa, maumivu ya nyonga)
ii) Vipimo vya maabara
Kipimo cha damu (CBC) – Kutathmini upungufu wa damu (anemia) au maambukizi
Kupima mimba (hCG) – Kuthibitisha au kubaini ujauzito
Vipimo vya homoni – FSH, LH, estrogeni, progesterone, androjeni
Vipimo vya magonjwa ya inzaa – Kuangalia uwepo wa maambukizi ya Klamidia, kaswende na kisonono
iii) Uchunguzi wa picha na uchunguzi maalum
Ultrasound ya nyonga – Kubaini uvimbe, cysts, au matatizo ya uterasi
Hysteroscopy – Kuchunguza moja kwa moja ndani ya mji wa mimba
Biopsy ya Endometrium – Kuchukua sampuli ya ukuta wa kizazi kutathmini saratani
Pap Smear na Kipimo cha HPV – Kuchunguza saratani ya shingo ya kizazi
Matibabu ya kutokwa na damu katikati ya hedhi
Matibabu ya kutokwa damu katikati ya mzunguko wa hedhi hutegemea chanzo cha tatizo, baadhi yake huhusisha:
Tiba ya Homoni – Vidonge vya uzazi wa mpango, tiba ya homoni (GnRH analogs) kwa matatizo ya homoni, PCOS, na endometriosis.
Antibiotiki – Kwa maambukizi ya magonjwa ya zinaa au PID.
Upasuaji – Kuondoa fibroid, vinundu, tishu za endometria (endometriosis), au uvimbe wa saratani (kuondoa kizazi au sehemu ya kizazi).
Mabadiliko ya mtindo wa maisha – Kula chakula bora, kudhibiti uzito, kupunguza msongo wa mawazo.
Kurekebisha matumizi ya dawa – Ikiwa dawa fulani zinachangia au ksuabababisha tatizo, mfano dawa za kuyeyusha damu.
Wakati gani unapaswa kumwona Daktari unapotokwa na damu katikati ya mzunguko wa hedhi?
Ni muhimu kutafuta msaada wa daktari ikiwa unapta hali na dalili zifuatazo;
Damu inatoka mara kwa mara katikati ya hedhi
Kutokwa na damu kunaambatana na maumivu makali ya nyonga, kizunguzungu, au homa
Unapata damu baada ya kufikia ukomo wa hedhi (komahedhi)
Kuna uchafu ukeni wenye harufu mbaya au maumivu baada ya tendo la ndoa
ULY CLINIC inakushauri uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba kabla ya kuchukua hatua yoyote ile baada ya kusoma majibu haya.
Kupata ushauri zaidi au tiba kutoka kwa daktari wa ULY CLINIC bofya hapa au tumia linki ya Pata tiba
Imeboreshwa,
21 Machi 2025, 07:22:34
Rejea za mada hii
Wise LA, Mikkelsen EM, Rothman KJ, Riis AH, Sorensen HT, Huybrechts KF, et al. A prospective cohort study of menstrual characteristics and time to pregnancy. American journal of epidemiology. 2011;174:701–9. doi: 10.1093/aje/kwr130.
Harlow SD, Ephross SA. Epidemiology of menstruation and its relevance to women’s health. Epidemiologic reviews. 1995;17:265–86. doi: 10.1093/oxfordjournals.epirev.a036193.
Direito A, Bailly S, Mariani A, Ecochard R. Relationships between the luteinizing hormone surge and other characteristics of the menstrual cycle in normally ovulating women. Fertility and sterility. 2013;99:279–85. doi: 10.1016/j.fertnstert.2012.08.047.
Chiazze L, Jr, Brayer FT, Macisco JJ, Jr, Parker MP, Duffy BJ. The length and variability of the human menstrual cycle. Jama. 1968;203:377–80.
Rowland AS, et al. Influence of medical conditions and lifestyle factors on the menstrual cycle. Epidemiology (Cambridge, Mass) 2002;13:668–74. doi: 10.1097/00001648-200211000-00011.
Mikolajczyk RT, Louis GM, Cooney MA, Lynch CD, Sundaram R. Characteristics of prospectively measured vaginal bleeding among women trying to conceive. Paediatric and perinatal epidemiology. 2010;24:24–30. doi: 10.1111/j.1365-3016.2009.01074.x.
Dasharathy SS, Mumford SL, Pollack AZ, Perkins NJ, Mattison DR, Wactawski-Wende J, et al. Menstrual bleeding patterns among regularly menstruating women. American journal of epidemiology. 2012;175:536–45. doi: 10.1093/aje/kwr356.
Livingstone M, Fraser IS. Mechanisms of abnormal uterine bleeding. Human reproduction update. 2002;8:60–7. doi: 10.1093/humupd/8.1.60.
Practice Committee of American Society for Reproductive Medicine. Myomas and reproductive function. Fertility and sterility. 2008;90:S125–30. doi: 10.1016/j.fertnstert.2008.09.012.
Taylor E, Gomel V. The uterus and fertility. Fertility and sterility. 2008;89:1–16. doi: 10.1016/j.fertnstert.2007.09.069.
Ferenczy A. Pathophysiology of endometrial bleeding. Maturitas. 2003;45:1–14. doi: 10.1016/s0378-5122(03)00068-9.
Heitmann RJ, Langan KL, Huang RR, Chow GE, Burney RO. Premenstrual spotting of >/=2 days is strongly associated with histologically confirmed endometriosis in women with infertility. American journal of obstetrics and gynecology. 2014;211:358.e1–6. doi: 10.1016/j.ajog.2014.04.041.