top of page

Utangulizi

​

Maumivu ya miguu wakati wa usiku, kwa jina jingine yakijulikana kama maumivu yanayohusiana na kulala huwa ni maumivu yanayotokea si kwa nadra na husababisha maumivu ambayo yanasababisha mtu kukosa usingizi. Maumivu haya hutokana na kukakamaa ghafla kwa misuri, hali hii huanza ghafla na hudhuru sana misuli ya vigimbi

Sehemu hii tunazungumzia maumivu ya miguu ya aina hii tu.

​

Epidemiolojiaya tatizo

​

Maumivu ya miguu wakati wa usiku hutokea sana kwa  wagonjwa lakini haya ripotiwi na wagonjwa kwa madaktari. Kwa kawaida hutokea kwa asilimia 40 kwa watu wenye umri zaidi ya miaka 50 na hutokea sana jinsi umri unavyoendelea.Tatizo hili husababisha matatizo mengi ya kukosa usingizi.

​

Tatizo hili huweza kutokea kwa watoto wadogo pia lakini kwa asilimia 7 tu haswa kwenye umri wa miaka 16 hadi 18.

​

Visababishi, dalili na matibabu

bottom of page