top of page

Mwandishi:

Mhariri:

Imeboreshwa:

Dkt. Charles W, MD

Dkt. Adolf S, M.D

2 Aprili 2026, 16:17:51

Maudhi ya PEP

Maudhi ya PEP ni madhara madogo yanayotokana na matumizi ya PEP. Mara nyingi unavuoanza kutumia PEP utaanza kuhisi na kuona mabadiliko mbalimbali mwilini mwako ambayo yataisha kwa jinsi siku zinavyoenda.


Maudhi ya PEP ni yapi?

Maudhi ya PEP yanayotokea hutegemea aina ya dawa inayotumika, katika sehemu hii utajifunza maudhi yanayotokea sana na yale ya nadra kwa mchanganyiko wa dawa zinazotumika ambazo ni;


1. Tenofovir EMT na Dolutegravir au na raltegravir


Na mbadala wake ambao huwa na mchanganyiko


2. Tenofovir EMT na darunavir (DRV)(800 mg) au na ritonavir


Kumbuka: Tenofovir EMT ni mchanganyiko wa tenofovir na Emtricitabin)


Maudhi makuu ya Tenofovir EMT
  • Kichefuchefu

  • Mvurugiko wa tumbo

  • Maumivu ya kichwa

  • Kizunguzungu

  • Udhaifu

  • Uchavu mkali



Maudhi ya nadra ya Tenofovir EMT
  • Matatizo ya figo

  • Kusinyaa kwa mifupa


Maudhi haya hutokea kama ikitumika kwa muda mrefu.


Maudhi makuu ya Dolutegravir
  • Kichefuchefu

  • Maumivu ya kichwa

  • Kuhara


Maudhi ya nadra ya Dolutegravir
  • Matatizo ya figo

  • Harara

  • Mzio wa dawa


Maudhi ya Darunavir
  • Maumivu ya kichwa

  • Kuhara

  • Kutapika

  • Maumivu ya tumbo

  • Haja ngumu


Maudi ya ritonavir
  • Usingizi mzito

  • Kuhara

  • Gesi tumboni

  • Kiungulia

  • Kubadilika kwa uwezo wa kutambua ladha

  • Maumivu ya kichwa

  • Gamzi, hisia za kuungua, kuchomachoma kwenye viganja vya mikono, miguu na midomo

  • Maumivu ya misuli au maungio ya mifupa

  • Kicefuchefu

  • Kutapika


Kwa ujumla maudhi yanayotokea hutegemea mchanganyiko wa dawa unazotumia, ili kufahamu zaidi kuhusu maudhi ya dawa ulizopewa, angalia maudhi katika kila dawa unayotumia.


Dalili kali za matumizi ya PEP

Kama ukipata dalili kali za matumizi ya PEP onana na daktari haraka iwezekanavyo. Miongoni mwa dalili hizo ni;


  • Harara kwenye ngozi

  • Kubabuka au kuungua ngozi

  • Vidonda kwenye midomo

  • Macho kuwa mekundi, kuvimba, kuwasha au kutokwa machozi

  • Maumivu ya misuli maungio ya mifupa

  • Homa

  • Kuvimba, maumivu au dalili za maambukizi

  • Kichefuchefu kikali

  • Uchovu mkali

  • Kukosa hamu ya kula

  • Maumivu upande wa kulia juu ya tumbo chini ya mbavu

  • Kinyesi kuwa cheusi au kilichopauka

  • Manjano machoni au kwenye ngozi

  • Kizunguzungu

  • Mapigo ya moyo kwenda tofauti na kawaida

  • Kizunguzungu

  • Kuoteza fahamu


Wapi unaweza kupata maelezo zaidi?

Unaweza kupata maelezo zaidi kwa kubofya katika makala zifuatazo:

Imeandikwa:

2 Aprili 2026, 16:17:51

ULY CLINIC inashauri usitegemee au kufuata ushauri wowote uliyoona kwenye makala hii bila kuwasiliana kwanza na daktari wako. Kabla ya kuchukua hatua yoyote ya matibabu, hakikisha umepata ushauri rasmi kutoka kwa daktari wako ili kuepuka madhara yoyote yanayoweza kutokea.

​

Makala hii ni ya kielimu tu na haitumiki kama mbadala wa matibabu ya daktari.

bottom of page