Mwandishi:
Mhariri:
Imeboreshwa:
ULY CLINIC
ULY CLINIC

6 Aprili 2026, 12:12:44
Bronkaitiz sugu
Ni zipi dalili za bronkaitisi sugu?
Bronkaitisi sugu ni aina ya ugonjwa sugu wa kuziba kwa njia ya hewa (COPD). Katika hali hii, matumizi ya misuli ya ziada kwa kupumua huwa ya muda mrefu na hutanguliwa na kikohozi chenye makohozi pamoja na kupumua kwa shida wakati wa shughuli.
Dalili zinazohusiana na bronkaitisi sugu ni:
Kifua kutoa miruzi (sauti ya juu wakati wa kupumua),
Krako (sauti inayosikika sehemu za chini),
Kupumua haraka haraka
Uvimbaji wa mishipa ya shingo (Jugula vena),
Muda mrefu wa kutoa pumzi
Kifua cha pipa
Kuvimba kwa vidole (kuwa mithiri ya rungu).
Ngozi na midomo kuwa buluu na kuongezeka uzito kutokana na uvimbe huchangia jina la kawaida la "Uvimbe wa blue" kwa wagonjwa wa bronkaitisi sugu. Homa ya kiwango cha chini inaweza kutokea iwapo kuna maambukizi upili
ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba zaidi kabla ya kuchukua hatua yoyote ile ya kiafya baada ya kusoma makala hii.
Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia namba za simu au kubonyeza link ya Pata Tiba chini ya tovuti hii
Imeandikwa:
2 Aprili 2026, 15:59:23
Soma dalili zingine Zaidi kwa kubonyeza herufi ya mwanzo hapa chini
​
[A] [B] [C] [D] [E] [F] [G] [H] [I] [J] [K] [L] [M] [N] [O] [P] [Q] [R] [S] [T] [U] [V] [W] [X] [Y] [Z] [Z] [#]
Rejea za mada
ULY CLINIC
