Mwandishi:
Mhariri:
Imeboreshwa:
ULY CLINIC
ULY CLINIC
6 Aprili 2026, 12:18:41
Maumivu wakati wa hedhi (Dysmenorrhea)
Dismenorrhea ni maumivu ya tumbo wakati wa hedhi, huathiri zaidi ya asilimia 50 ya wanawake walio kwenye kipindi cha kuona hedhi.
Maumivu haya huweza kuja na kuondoka, kuwa butu au ya kuchoma kama mshale. Mara nyingi huambatana na maumivu makali ya kunyonga au kubana yanayosambaa kuelekea kwenye njia ya haja kubwa au mapajani, na huweza kutangulia kabla ya kuona damu au wakati damu inatoka.
Visababishi
Adenomysosis
Kusinyaa kwa tundu la shingo ya kizazi
Endometriosis(kutungishwa cha chembe za endometria nje ya mfuko wa kizazi)
Magonjwa ya michomo kwenye nyonga (PID)
sindromu ya komahedhi
Maumivu yasiyokuwa nasababu za awali
Fibraoid ndani ya mfuko wa kizazi
Matumizi ya vipandikizi vinavyowekwa ndani ya kizazi
ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba zaidi kabla ya kuchukua hatua yoyote ile ya kiafya baada ya kusoma makala hii.
Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia namba za simu au kubonyeza link ya Pata Tiba chini ya tovuti hii
Imeandikwa:
2 Aprili 2026, 15:59:23
Soma dalili zingine Zaidi kwa kubonyeza herufi ya mwanzo hapa chini
​
[A] [B] [C] [D] [E] [F] [G] [H] [I] [J] [K] [L] [M] [N] [O] [P] [Q] [R] [S] [T] [U] [V] [W] [X] [Y] [Z] [Z] [#]
Rejea za mada
