top of page

Mwandishi:

Mhariri:

ULY CLINIC

Dkt. Benjamin L, MD

6 Novemba 2024, 12:19:44

Maumivu ya uke wakati wa tendo
shahawa-zenye-damu-ulyclinic-compressor.

Maumivu ya uke wakati wa tendo

Disparunia ni neno la tiba linalotumiwa na ULY clinic, neno hili limetokana na neno tiba disypareunia ambalo pia lilitokana na neno la kiingereza “dys”- ugumu na neno la kigiriki “pareunos” wa kulalala na mwenza.

Hivyo neno disparunia maana yake ya awali ni ugumu wa kulala kimwili na mwenza au maumivu ya uke wakati wa kujamiiana au maumivu wakati wa tendo la ndoa.

Maumivu makali ya uke wakati wa kujamiiana au kujisafisha huweza sababishwa na mambo mbalimbali ikiwa pamoja na aina ya maumbile, hali ya uke na magonjwa. Sababu za hali ya uke huwa pamoja na uke uliokauka au kutokuwa na majimaji ya kutosha wakati wa tendo ambapo huweza kutokana na matumizi ya dawa aina fulani au udhaifu wa kutozalisha kiwango sahihi cha homoni za kike kwenye damu.

 

Dalili na viashiria


Dalili na viashiria vya maumivu makali wakati wa ngono huwa pamoja na

  • Kupata maumivu wakati uume unaingia

  • Kupata maumivu mara zote uume unapoingia au unapojisafisha

  • Kupata maumivu makali wakati uume unapoingia na kutoka wakati wa tendo

  • Kupata maumivu ya kuungua au kuchoma

  • Kupata maumivu ya kupwita pwita.

Visababishi

Visababishi vya maumivu makali ya uke wakati wa uume au kitu kigeni kinaingia ukeni ni pamoja na:

Kutokuwa na ute wa kutosha ukeni

Kwa kutoandaliwa vema wakati wa tendo la kujamiiana, kutokuwa na hisia za tendo au mabadiliko ya homoni kama yanayotokea kwa wanawake wanaoelekea kwenye umri wa komahedhi au walio kwenye komahedhi husababisha majimaji ya uke kuwa kidogo na kupelekea maumivu ya uke.


Matumizi ya dawa za aina fulani

Pia huweza kusababisha kupunguza hamu ya tendo na maji ya uke. Dawa hizi ni pamoja dawa za magonjwa ya akili (antidepressant), dawa za kushusha presha, dawa jamii ya sedativi, dawa za jamii ya antihistamini na dawa za kumeza za uzazi wa mpango.


Majeraha

Majeraha kwenye uke yanaweza kutokana na ajali, upasuaji wa nyonga, ukeketaji, au kuongezewa njia ya uke wakati wa kjifungua.

Michomo, maambukizi na matatizo ya Ngozi

Maambukizi kwenye uke au magonjwa ya Ngozi ya uke yanaweza kukusababishia maumivu wakati wat endo la kujamiana

Vajinizimu- hutokana na misuli ya uke kubana kwa muda mrefu pasipokuachia pasipo lazima, hali hii huleta maumivu makali sana wakati wa tendo.

Madhaifu ya kuzaliwa nayo

Matatizo ya kuzaliwa ambayo huonekana sana utotoni, kutokuwa na uke au kuwa na uke nusu au kuwa na ukuta wa bikra (haimen). (ukuta unaoziba kitu chochote kuingia kwenye uke) au kizazi kilichokaa vibaya huweza kusababisha maumivu ya uke.

Maumivu makali kwenye kilele cha uke

Maumivu ya ndani hutokea endapo uume umezama ndani kabisa. Maumivu haya huweza kuwa makali zaidi kutegemea pozi la wakati wa tendo. Visababishi vya maumivu haya huwa ni aina fulani ya magonjwa na hali kama vile uvimbe wa faibroidi, adenomayosisi, uvimbe maji kwenye ovari na bawasili, sindromu matumbo korofi na udhaifu kwenye sakafu ya nyonga. Sababu zingine ni ugonjwa wa Michomokinga kwenye nyonga, maambukizi kwenye vifuko maji ndani ya ovari na endometriosisi.


Upasuaj na dawa unaweza kuchangia pamojakama upasuaji wa kuondolewa kizazi, na dawa za kemotherapi na mionzi.

Matatizo ya hali ya moyo

Maumivu wakati wa kujamiana huweza kusababishwa na magonjwa ya kisaikolojia kama ugonjwa wa Ang’zayati, dipresheni, hofu ya kuogopa mahusiano, msongo wa mawazo, magonjwa ya somataizesheni n.k.

Hata hvyo kufanyiwa ukatili wa kijinsia unaweza kuchangia maumivu wakati wa tendo, ikumbukwe tafiti zinaonyesha si kila mwanamke aliyepata ukatili wa kijinsia hupata tatizo la maumivu wakati wa tendo.

Jedwali 1: Baadhi ya visababishi vya maumivu wakati wa Tendo la ndoa kwa mwanamke

Sababu

Maelezo ya Chanzo

Dalili Kuu

Mapendekezo ya Matibabu ya Nyumbani

Ukavu wa uke

Ukosefu wa ute ukeni kutokana na homoni, msongo wa mawazo, au hamasa hafifu.

Maumivu ya kuchoma, kukwaruza, maumivu mwanzoni mwa tendo.

Tumia vilainishi (water-based), ongeza muda wa hamasa, epuka sabuni zenye kemikali.

Maambukizi ya ukeni (fangasi, BV, zinaa)

Fangasi, bakteria au magonjwa ya zinaa yanayoshambulia uke au shingo ya kizazi.

Kuwashwa, harufu mbaya, uchafu wa rangi isiyo ya kawaida, maumivu wakati wa tendo.

Tumia dawa za fangasi (OTC), epuka “kujitakasa ukeni”, vaa nguo za pamba.

Endometriosis

Ukuaji wa tishu ya endometrium nje ya mji wa mimba; husababisha uvimbe na maumivu.

Maumivu ya kina wakati wa tendo, hedhi chungu, maumivu ya tumbo ya mara kwa mara.

Tumia dawa za kupunguza maumivu (NSAIDs), andika dalili zako, muone daktari kwa uchunguzi zaidi.

Hofu au msongo wa mawazo (vajinizimu ya hofu)

Hali ya kisaikolojia inayosababisha misuli ya uke kukakamaa bila hiari.

Maumivu ya ghafla, uke kubana kupita kiasi, kushindwa kufurahia tendo.

Mazungumzo ya wazi na mwenzi, mazoezi ya kupumzika, ushauri wa kitaalamu).

Jeraha la uke (baada ya kujifungua, upasuaji)

Mishono, kovu, au tishu kupona vibaya baada ya kujifungua au upasuaji.

Maumivu ya sehemu ya chini, hasa wakati uume unagusa sehemu yenye kovu.

Tumia vilainishi, subiri kupona kabisa, chagua mikao isiyo na msuguano mkubwa.

Faibroid au uvimbe kwenye kizazi

Uvimbe wa kawaida wa kizazi unaoweza kushinikiza njia ya uke au viungo vya karibu.

Maumivu ya kina wakati wa tendo, hedhi nzito au ndefu, shinikizo kwenye nyonga.

Punguza maumivu kwa NSAIDs, jadiliana na daktari kuhusu ultrasound.

Uambukizi wa njia ya mkojo (UTI)

Maambukizi kwenye kibofu cha mkojo au urethra, yanayosababisha ukakasi.

Maumivu wakati wa kukojoa, shinikizo kwenye tumbo la chini, maumivu wakati wa tendo.

Kunywa maji mengi, epuka kuchelewa kukojoa, tumia dawa ya kuua bakteria iwapo inawezekana.

Mabadiliko ya homoni (komahedhi, kunyonyesha)

Kupungua kwa estrojeni hufanya uke kuwa mwembamba na mkavu (kusinyaa kuta za uke).

Ukavu, kuchoma, kupungua kwa ute wa ukeni, maumivu ya mara kwa mara.

Tumia vilainishi, ulizia daktari kuhusu krimu za estrojeni za kujipaka.


Matibabu ya maumivu makali ya uke wakati wa ngono

Matibabu yataanza na vipimo kisha kupewa tiba kulingana na visababishi vilivyofahamika. Endapo unatatizo la kisaikolojia, daktari wa saikolojia atakuwa nawe kukushauri katika darasa maalumu ili urejee kwenye hali ya kawaida. Kuhusu matibabu zaidi soma kwenye jedwali namba 1 hapo juu.


Hitimisho

Maumivu wakati wa tendo la ndoa kwa mwanamke si jambo la kawaida, wala si hali ya kuvumilia kimyakimya. Ni dalili muhimu inayoweza kuashiria matatizo ya kiafya, kihisia, au kisaikolojia. Kwa kutambua dalili mapema na kuchukua hatua sahihi- ikiwa ni pamoja na mawasiliano ya wazi na mwenzi, matumizi ya tiba za nyumbani, na kufuata ushauri wa kitaalamu — matatizo haya yanaweza kutibiwa na maisha ya ndoa kurejea katika hali ya furaha na starehe.

Kumbuka:

  • Hakuna sababu ya aibu kutafuta msaada.

  • Mawasiliano baina ya wanandoa ni silaha ya kwanza ya uponyaji.

  • Na mwisho, mtaalamu wa afya yupo kusaidia, si kuhukumu — usisite kumwona unapohisi haja.


Majina mengine ya makala hii

Makala hii huwa na majina mengine yafuatayo yanayomaanisha maumivu ya uke wakati wa kujamiana

  • Maumivu ya uke wakati wa kujamiana

  • Maumivu ya uke wakati wa kuingiza uume

  • Maumivu ya uke wakati wa kufika kileleni

  • Maumivu ya uke wakati wa ngono

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba zaidi kabla ya kuchukua hatua yoyote ile ya kiafya baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia namba za simu au kubonyeza link ya Pata Tiba chini ya tovuti hii

Imeboreshwa, 

30 Mei 2025, 12:46:52

Soma dalili zingine Zaidi kwa kubonyeza herufi ya mwanzo hapa chini

[A] [B] [C] [D] [E] [F] [G] [H] [I] [J] [K] [L] [M] [N] [O] [P] [Q] [R] [S] [T] [U] [V] [W] [X] [Y] [Z] [Z] [#]

Rejea za mada

Kingsberg S, et al. Approach to the woman with sexual pain. https://www.uptodate.com/contents/search. Imechukuliwa 17.04.2020

Frequently asked questions. Gynecologic problems FAQ020. When sex is painful. American College of Obstetricians and Gynecologists. https://www.acog.org/Patients/FAQs/When-Sex-Is-Painful.Imechukuliwa 17.04.2020

Dyspareunia. Merck Manual Professional Version. https://www.merckmanuals.com/professional/gynecology-and-obstetrics/sexual-dysfunction-in-women/dyspareunia?qt=dyspareunia&alt=sh. Imechukuliwa 17.04.2020

Barbieri R. Differential diagnosis of sexual pain in women. https://www.uptodate.com/contents/search. Imechukuliwa 17.04.2020

Kellerman RD, et al. Female sexual dysfunction. In: Conn's Current Therapy 2019. Elsevier; 2019. https://www.clinicalkey.com. Imechukuliwa 17.04.2020

Faubion SS, et al. Genitourinary syndrome of menopause: Management strategies for the clinician. Mayo Clinic

Ospemifene oral. Facts & Comparisons eAnswers. http://fco.factsandcomparisons.com/lco/action/search?q=Ospemifene%20oral&t=name&va=Ospemifene%20oral.Imechukuliwa 17.04.2020

Sauer U, et al. Efficacy of intravaginal dehydroepiandrosterone (DHEA) for symptomatic women in the peri- or postmenopausal phase. Maturitas. 2018; doi:10.1016/j.maturitas.2018.07.016.

bottom of page