top of page

Mwandishi:

Mhariri:

Dkt. Benjamin l, MD

Dkt. Peter A, MD

24 Desemba 2021, 09:44:59

Maumivu ya hedhi
shahawa-zenye-damu-ulyclinic-compressor.

Maumivu ya hedhi

Maumivu wakati wa hedhi kwa jina la tiba linalotumiwa na ulyclinic ni "dismenorea". Neno hili limetoholewa kutoka neno tiba "Dysmenorrhea" ambalo lina asili ya maneno ya Kigiriki na Kilatini

Dismenorea ni maumivu ya kubana au kuchoma yanayotokea kabla au wakati wa damu ya hedhi.


Maumivu yoyote yale ya hedhi huamshwa na kemikali zinazoitwa prostaglandin na leukotriene katika mfumo wa uzazi ambazo ni kawaida kuzalishwa wakati wa yai kutengenezwa na kutoka kwenye ovari.

Kiwango hiki huongezeka sana kwenye kipindi cha yai kutolewa kutoka katika ovari na wakati ukuta wa ndani ya mfuko wa kizazi unapoanza kuvunjika endapo uchavushwaji wa Yai haujatokea.


Kemikali hizi husababisha mfuko wa uzazi kubana na kuachia ili kutoa kuta zilizojengwa kwa muda wa siku 28 au 31 endapo tu yai lililotoka kwenye ovari halikuchavushwa. Ukuta huu unapovunjika hutoa dalili za damu ya kila mwezi, ukuta mwingine hujengwa tena baada ya damu ya mwezi kutatika.

Visababishi


Kuna aina mbili za maumivu ya hedhi Aina ya awali na aina ya sekondari.


Aina ya awali imezungumziwa hapa, kwa jina jingine hujulikana kama maumivu ya kawaida wakati wa hedhi na hutokea mwaka mmoja (1) au miwili baada ya mwanamke kuvunja ungo. Mwanamke hupata maumivu ya tumbo la chini ya kitovu au mgongoni.


Maumivu ya hedhi ya kawaida maranyingi huanza muda mfupi kabla mwanamke hajaanza kuona damu ya hedhi, hudumu muda wa siku tatu au pungufu. Maumivu hupungua siku zinavyoendelea na kuisha kabisa.


Dalili zake ni zipi?


Maumivu ya kubana chini ya kitovu na nyonga yanayoelekea kwenye;

Mapaja na

Mgongo


Endapo dalili zimekuwa mbaya zaidi mwanamke anaweza kupata;

  • Mvurugiko wa tumbo

  • Wakati mwingine kutapika

  • Kupata choo laini au

  • Kuharisha


Maumivu ya hedhi aina ya sekondari


Kwa wanawake wenye maumivu makali ya kupindukia asilimia 10 huwa na uvimbe usio saratani kwenye mfuko wa kizazi au kuwa na chembe hai za ndani ya mfuko wa kizazi nje ya mfuko wa ya kizazi huitwa kwa jina la tiba endometriosisi


Aina ya sekondari husababishwa na mabadiliko au magonjwa yaliyo katika kizazi kama vile tatizo la endometriosisi (kuwepo kwa ukuta wa ndani ya kizazi nje ya kizazi maeneo ya mirija ya uzazi, kibofu, nje ya ukuta wa kizazi, sehemu ya haja kubwa, kiwanda cha ovari)


Tatizo la endometriosis husababisha damu ya hedhi kuvilia kwenye ogani zilizo ndani ya nyonga, michomo na makovu nje ya mfumo wa kizazi na ogani zilizo ndani ya nyonga hutokea hivyo husababisha maumivu pengine yanayouma muda mrefu na yasiyo isha.


Visababishi

Maumivu ya hedhi mara chache husababishwa na;


  • Madhaifu/ugonjwa ndani ya nyonga (matatizo ya kuzaliwa ya mfuko wa uzazi).

  • Endometriosis

  • Ugonjwa wa michomo kwenye mfuko wa uzazi (Ugonjwa wa Pelvic inflammatori (PID)

  • Uvimbe kwenye mfuko wa kizazi (fibroids)

Nitafanya nini kutibu tatizo hili la maumivu makali ya hedhi?

Tiba zipo kuweza kutuliza maumivu yasiyo makali sana kwa kutumia dawa ya asprini au dawa zingine za kutuliza maumivu, itakupasa kunywa dawa mara utakapoanza kuona siku zako.

Kuoga maji ya moto au kujikanda kwa maji ya moto maeneo ya tumbo la chini na mgongoni kunaweza kusaidia kupunguza maumivu.


Kama maumivu ni makali zaidi

  • Pata muda wa kupumzika

  • Acha kunywa pombe

  • Acha vyakula vyenye caffeine au chumvi maana huongeza misuli kubana na kuachia na hivo kuleta maumivu

  • Kanda tumbo na mgongo

  • Pia fanya mazoezi kwa mujibu wa ratiba yako kwa maana tafiti zinaonesha kuwa mazoezi hupunguza maumivu ya hedhi na hufupisha siku za kuona damu. Hata hivyo kujamiiana wakati wa hedhi kunaweza kupunguza maumivu ya hedhi pia


Endapo maumivu yamezidi sana

  • Kunywa dawa zenye nguvu zaidi kama utavyoshauliwa na dakitari

  • Unaweza ukatumia dawa za uzazi wa mpango


Wakati gani upate msaada kutoka kwa daktari?


  • Kwa wanawake wengi baadhi ya maumivu wakati wa hedhi ni jambo la kawaida, hata hivyo unabidi kuwasiliana na daktari wako endapo;

  • Dawa jamii ya NSAIDS na matibabu yasiyo dawa hayajakusaidia kabisa

  • Maumivu ya hedhi yamekuwa makali Zaidi ghafla

  • Una Zaidi ya miaka 25 na umepata maumivu ya hedhi makali sana kwa mara ya kwanza

  • Maumivu ya hedhi yameambatana na homa

  • Unapata maumivu ya hedhi hata kama huoni damu ya hedhi(piriodi)


Utajuaje maumivu yako ni ya kawaida?


Kama unapata maumivu yanayozidi siku tatu na ni makali basi onana na dakitari maana matatizo haya hutibika hospitali endapo wataona kinachosababisha ni nini. Pia unaweza kusoma kuhusu tiba asilia namaumivu ya hedhi kwa kubonyeza hapa.


ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba zaidi kabla ya kuchukua hatua yoyote ile ya kiafya baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia namba za simu au kubonyeza link ya Pata Tiba chini ya tovuti hii

Imeboreshwa, 

24 Desemba 2021, 09:52:22

Soma dalili zingine Zaidi kwa kubonyeza herufi ya mwanzo hapa chini

[A] [B] [C] [D] [E] [F] [G] [H] [I] [J] [K] [L] [M] [N] [O] [P] [Q] [R] [S] [T] [U] [V] [W] [X] [Y] [Z] [Z] [#]

Rejea za mada

1. Hassan Nagy, et al. Dysmenorrhea. https://www.ncbi.nlm.nih.gov/books/NBK560834/.Imechukuliwa 24.12.2021

2. Bernardi, et al. “Dysmenorrhea and related disorders.” F1000Research vol. 6 1645. 5 Sep. 2017, doi:10.12688/f1000research.11682.1

3.Period pain.https://www.ncbi.nlm.nih.gov/books/NBK279324/. Imechukuliwa 24.12.2021.

4. Proctor, et al. “Diagnosis and management of dysmenorrhoea.” BMJ (Clinical research ed.) vol. 332,7550 (2006): 1134-8. doi:10.1136/bmj.332.7550.1134

bottom of page