top of page

Mwandishi:

Mhariri:

ULY CLINIC

Dkt. Sospeter B, MD

15 Januari 2021, 13:59:06

Mwili kuchoka
shahawa-zenye-damu-ulyclinic-compressor.

Mwili kuchoka

Uchovu wa mwili hufahamika kitiba kama body malaise, uchovu mkali wa mwili hufahamika kama fatigue. Maneno haya mawili hutumika kumaanisha vitu viwili tofauti, hata watu wengi wamekuwa wakitumia maneno haya kwa kubadilishana.


Fatigue ni ugumu wa mwili katika kuanza au kuendelea kufanya kazi, mfano unashindwa kuanza kutembea au kuendelea kutembea kwa sababu mwili hauwezi kufanya hivyo. Wakati huu utakuwa unapata dalili ya mwili wako kuwa mzito sana. Kwa maana nyingine fatigue huwa ni uchovu mkali wa mwili unaoambatana na dalili zingine za hofu, kushindwa kufanya kazi, kushindwa kufikiria vema na kutulia kimawazo na kukosa mzuka wa kufanya kazi


Body malaise ni hali ya ujumla ya mwili kutojihisi vema inayoambatana na kutokuwa vema katika afya.


Maneno haya yote mawili huwa tofauti na neno lilaloitwa kuchoka, hata hivyo watu hulitumia vibaya neno kuchoka wakimaanisha fatigue au body malaise. Kuchoka ni hali ya mwili kushindwa kuendelea kufanya kazi baada ya kuwa umefanya kazi kwa kipindi Fulani.


Uchovu wa mwili husababishwa na nini?


Uchovu wa mwili huwa ni dalili ya kitu fulani kinachoendelea ndani ya mwili, inaweza kuwa kiashiria cha kuchoka tu kawaida mara baada ya kufanya kazi au uchovu ambao unasababishwa na ugonjwa.


Visababishi vya kuchoka mwili vimegawanyika katika makundi matatu, vile vinavyosababisha tatizo la hivi karibuni, au tatizo la ndani ya miezi sita au tatizo sugu yaani zaidi ya miezi sita.


Visababishi vya tatizo lisilo sugu

  • Upungufu wa damu mwilini

  • Maudhi makubwa ya dawa

  • Msongo wa mawazo au sonono


Visababishi vya tatizo lisilo sugu

Visababishi vya tatizo lisilo sugu ni;


  • Ugonjwa wa Kisukari

  • Kuugua saratani

  • Upungufu wa homoni za thyroid (Hypothyroidism)

  • Kutolala vema usiku


Visababishi vya tatizo sugu

Visababishi vya tatizo sugu ni;


  • Uvimbe wa maambukizi kwenye ubongo

  • Msongo wa mawazo

  • Matumizi ya dawa kwa muda mrefu mfano dawa za kutibu degedege na kifafa, dawa za aleji jamii ya antihistamine, dawa za kutibu shinikizo la juu na magonjwa ya moyo, dawa za magonjwa ya akili

  • Magonjwa ya mapafu na moyo

  • Ugonjwa wa obeziti

  • Magonjwa sugu mwilini


Visababishi

  • Kutopata usingizi

  • Matumizi ya pombe ya kupindukia

  • Kutokula mlo kamili

  • Kunywa kahawa kwa wingi

  • Kutofanya mazoezi au kuushughulisha mwili wako


Dalili zinazohitaji uchunguzi wa haraka


Endapo dalili zifuatazo zimeambatana na uchovu wa mwili unahitaji kufanyiwa uchunguzi wa haraka.


Dalili hizo ni;


  • Tatizo endelevu la kupungua uzito

  • Homa ya muda mrefu au kutokwa na jasho wakati wa usiku

  • Kuvimba kwa mitoki maeneo mengi ya mwili

  • Kupooza kwa misuli au kukosa hisia

  • Kukohoa damu

  • Kutapika damu

  • Kuishiwa pumzi

  • Tumbo kujaa maji

  • Kukanganyikiwa (confusion)

  • Hisia za kutaka kujiua

  • Kupata maumivu ya kichwa mapya au kuzidi


Vipimo


Vipimo vitakavyoombwa na daktari vitategemea ameona tatizo lako ni nini; vipimo vinaweza kuagizwa kutegemea pia na dalili zingine ambazo unazo ambavyo vinaweza kuwa kati ya;


Kipimo cha FBP

Kupima kiwango cha Ferritin

Kipimo cha Erythrocyte sedimentation rate (ESR)

Kipimo cha Thyroid-stimulating hormone (TSH)

Kipimo cha serum electrolytes,

Kipimo cha serum glucose

Kipimo cha kuangalia utendaji kazi wa figo (Renal function test)

Kipimo cha kuangalia utendaji kazi wa Ini (liver function test)


Matibabu ya hospitali


Mara nyingi matibabu huelekezwa kutibu kisababishi, baada ya kuchukuliwa historia ya tatizo lako na kufanyiwa vipimo daktari anaweza kutambua shida yako kisha kupatiwa matibabu yanayokufaa.


Matibabu ya nyumbani

  • Wakati unasubiria kupata matibabu ya hospitali unaweza kufanya mambo yafuatayo ili kukuwezesha kupunguza hali ya kujihisi mchovu.

  • Fanya mazoezi, zingatia ushauri wa mazoezi kulingana na hali yako ya kiafya. Ingia katika kurasa za mazoezi ndani ya tovuti ya ULY CLINIC kusomo Zaidi.

  • Usilale muda mrefu wakati wa mchana. Kulala wakati wa mchana kunaweza kukufanya uchoke Zaidi na hivyo ukashindwa kulala vema wakati wa usiku. Kutolala vema wakati wa usiku hupelekea tatizo la kuhisi mwili mchovu kwa siku inayofuatia.

  • Acha kuvuta tumbaku au mazao yatokanayo na tumbaku kama sigara n.k ili kuzuia kupata magonjwa ya moyo, shinikizo la juu la damu na saratani

  • Kula mlo kamili wenye matunda kwa wingi na mboga za majani, usile vyakula vyenye mafuta kwa wingi au vyakula vya kukaangwa

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba zaidi kabla ya kuchukua hatua yoyote ile ya kiafya baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia namba za simu au kubonyeza link ya Pata Tiba chini ya tovuti hii

Imeboreshwa, 

19 Julai 2023, 19:54:12

Soma dalili zingine Zaidi kwa kubonyeza herufi ya mwanzo hapa chini

​

[A] [B] [C] [D] [E] [F] [G] [H] [I] [J] [K] [L] [M] [N] [O] [P] [Q] [R] [S] [T] [U] [V] [W] [X] [Y] [Z] [Z] [#]

Rejea za mada

1.Jameson JL, et al., eds. Fatigue. In: Harrison's Principles of Internal Medicine. 20th ed. McGraw Hill; 2018. https://accessmedicine.mhmedical.com. Imechukuliwa 14.01.2021
2.Heine M, et al. Exercise therapy for fatigue in multiple sclerosis. Cochrane Database of Systematic Reviews. http://ovidsp.tx.ovid.com/sp-3.18.0b/ovidweb.cgi. Imechukuliwa 14.01.2021
3.Ferri FF. Chronic fatigue syndrome. https://www.clinicalkey.com. Imechukuliwa 14.01.2021
4.Fatigue and traumatic brain injury. www.archives-pmr.org. Imechukuliwa 14.01.2021
5.Fatigue . https://www.msdmanuals.com/professional/special-subjects/nonspecific-symptoms/fatigue. Imechukuliwa 14.01.2021. Imechukuliwa 14.01.2021
6.Cancer treatment side effects. National Cancer Institute. htpp://www.cancer.gov/about-cancer/treatment/side-effects. Imechukuliwa 14.01.2021

bottom of page