top of page

Ugonjwa na dawa

Kurasa hii utajifunza kuhusu dawa na ugonjwa unaotibiwa na dawa hiyo. Wasiliana na daktari wako kabla ya kutumia dawa yoyotee ile ili kuepuka madhara na usugu wa dawa mwilini mwako. Kumbuka siku zote kuwa dawa ni sumu kwenye mwili wako endapo haitatumika bila ushauri wa daktari

Dawa ya kukojoa kitandani kwa watoto

Dawa ya kukojoa kitandani kwa watoto

Dawa zilizoruhusiwa na FDA/TMDA kuzuia tatizo la kukojoa kitandani kwa watoto ni dawa ya imipramine ambayo ni dawa ya kuzuia sonona na dawa inayofanya kazi kama homoni iitwayo desmopressin acetate.

Dawa ya homa ya ini

Dawa ya homa ya ini

Dawa ya homa ya ini katika makala hii, ni dawa ambazo zinatumika kutibu maambukiziya virusi vya homa ya ini aina B na C. Baadhi ya dawa zilizoorodheshwa hazipatikani katika baadhi ya nchi.

Dawa za kutibu kusinyaa kwa ini

Dawa za kutibu kusinyaa kwa ini

Dawa za kutibu ini lililosinyaa au kusinyaa kwa ini, katika Makala hii imemaanisha dawa zenye uwezo wa kupunguza au kuondoa dalili zinazotokana na ini kufeli kufanya kazi.

Dawa ya miguu kuwaka moto

Dawa ya miguu kuwaka moto

Miguu kuwaka moto katika Makala hii inajumuisha pia tatizo la kanyagio kuwaka moto, ambalo huelezewa kuwa ni hisia za joto, kuchomachoma kwa miguu, au kanyagio. Hali hii huweza kutokea wakati wa usiku au wakati wote haswa kwa watu wa makamo lakini haimaanishi kuwa haiwezi kutokea kwa watu walio na umri mdogo. Makala hii imezungumzia kuhusu dawa za tatizo la miguu kuwaka moto, kusoma zaidi kuhusu tatizo la miguu kuwaka moto, dalili na uchunguzi, nenda kwenye makala nyingine ndani ya tovuti ya ulyclinic.

Dawa za kutoa mimba

Dawa za kutoa mimba

Kutoa mimba ni kitendo cha kukatisha maisha ya kijusi aliyepo tumboni, hii inaweza kufanyika kwa kutumia dawa au kutumia njia ya upasuaji mdogo au kusafisha kizazi.

bottom of page