top of page

Mwandishi:

Mhariri:

Dkt. Peter R, CO

Dkt. Mangwella S, MD

Jumamosi, 4 Desemba 2021

Ubuyu
Ubuyu

Wataalamu wa afya wanautizama ubuyu kama tiba na chakula cha chembe hai za binadamu kwani umekua na faida nyingi sana kutokana na uwepo wa virutubisho muhimu kwa afya. Tunda hili hufahamika kuwa moja ya tunda lenye kiwango kikubwa cha viuasumu, matumizi yake ya mara kwa mara hukinga magonjwa sugu kama magonjwa ya moyo, mishipa ya damu na saratani.


Unaweza kupata wapi ubuyu?


Ubuyu pia unapatikana sehemu mbalimbali kama kwenye masoko, supamaketi, mpaka mitaani.


Viinilishe vinavyopatikana kwenye ubuyu


  • Mafuta

  • Madini

  • Vitamini

  • Protini

  • Nyuzilishe

  • Kabohaidreti

  • Maji


Viinilishe katika gramu 100 za ubuyu


Gramu 100 za ubuyu huwa na;


  • Nishati = 250kcal

  • Kabohaidreti = 80g

  • Protini = 3.7g

  • Nyuzilishe = 45g

  • Maji = 11g

  • Mafuta = 0.5g

  • Sukari = 4.7g


Madini katika gramu 100 za ubuyu


Gramu 100 za ubuyu huwa na;


  • Kalishiamu = 342mg

  • Madini Chuma = 8.4mg

  • Magineziamu = 158mg

  • Phosifolasi = 47mg

  • Potashiamu = 2189mg

  • Sodiamu = 10mg

  • Zinki = 1mg


Vitamini katika gramu 100 za ubuyu


Gramu 100 za ubuyu huwa na;


  • Vitamini B1 = 0.03mg

  • Vitamini B2 =0.074mg

  • Vitamini B3 = 20mg

  • Vitamini B6 = 2.4mg

  • Vitamini C = 173mg


Kemikali muhimu kwenye ubuyu


Ubuyu huwa na kiasi kikubwa cha antioxidants na polyphenol zinazosaidia kuzuia na kudhibiti magonjwa ya moyo, shambulio binafsi la mfumo wa kinga, kisukari na saratani.


Faida za ubuyu


Kula ubuyu husaidia;


  • Kuongeza hamu ya kula

  • Kupunguza uzito

  • Kusawazisha kiwango cha sukari mwilini

  • Kuimarisha na kuboresha mfumo wa mmeng`enyo wa chakula

Imeboreshwa,
4 Desemba 2021, 17:26:34
Bofya hapa kusoma zaidi kuhusu namna ya kuandaa vyakula mbalimbali vinavyoweza kukukinga dhidi ya magonjwa ya shinikizo la damu la juu na Kisukari, pia kuupa mwili wako uwezo wa kudhibiti magonjwa ya kisukari na shinikizo la juu la damu(presha).

 

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba zaidi kabla ya kuchukua hatua yoyote ile ya kiafya baada ya kusoma makala hii.
 

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kutumia namba za simu au kubonyeza link ya Pata Tiba chini ya tovuti hii

Rejea za mada hii

  1. Osman, M. A. (2004). "Chemical and nutrient analysis of baobab (Adansonia digitata) fruit and seed protein solubility". Plant Foods Hum Nutr. 59 (1): 29–33.

  2. Gardner, et al. May (2011). Heritage Trees of Penang. Penang: Areca Books. ISBN 978-9-675-71906-6.

  3. Adrian Patrut et al. (2018) The demise of the largest and oldest African baobabs. Nature Plants 4: 423–426.

  4. Rahul J, et al. Adansonia digitata L. (Baobab): A review of traditional information and taxonomic description. Asian Pac. J. Trop. Biomed. 2015;5:79–84.

  5. Ghoneim M.A, et al. Protective effect of Adansonia digitata against isoproterenol-induced myocardial injury in rats. Anim. Biotechnol. 2016;27:84–95.

  6. Vertuani S, et al. Antioxidant capacity of Adansonia digitata fruit pulp and leaves. Acta Phytother. 2002;V:2–7.

  7. Braca, Alessandra et al. “Phytochemical Profile, Antioxidant and Antidiabetic Activities of Adansonia digitata L. (Baobab) from Mali, as a Source of Health-Promoting Compounds.” Molecules (Basel, Switzerland) vol. 23,12 3104. 27 Nov. 2018, doi:10.3390/molecules23123104

bottom of page