Huduma ya kwanza
Katika sehemu hii utajifunza kuhusu huduma ya kwanza kwenye matukio mbalimbali ili uweze kuwa msaada pale itakapohitajika kabla wataalamu wa afya hawajafika kwenye tukio

Mdudu sikioni- Huduma ya kwanza
Mdudu kuingia masikioni ni jambo linaloweza kutokea kwa kila mtu. Muda muafaka huweza kuwa wakati umekaa mchana au wakati umelala usiku. Wadudu wanaoweza kuingia sikioni ni mbu, nzi, mende na wengine. Mdudu anaweza kuingia sikioni na akaishi muda mrefu au akafia ndani bila wewe kufahamu.

Kiharusi-Huduma ya kwanza
Ubongo wa binadamu unahitaji kupata hewa safiya oksijeni pamoja na sukari ya glucose muda wote ili uweze kufaya kazi yake vema, vitu hivi viwili hupelekwa kwenye ubongo kupitia damu. Kiharusi kinaweza kutokea endapo damu haiwezi fika vema eneo fulani la ubongo, hii husababisha kukosa oksijen na sukari hivyo kufa na kupelekea kuonekana kwa dalili za kiharusi. Endapo mtu amepata kiharusi, kitu cha pekee unachoweza kufanya ni kumsaidia kuweza kuzuia eneo kubwa la ubongo kuathirika kwa kukosa damu.

Presha ya kupanda -Huduma ya kwanza
Kurasa hii imezungumzia kuhusu huduma ya kwanza kwa mgonjwa mwenye shinikizo la juu la damu au presha ya kupanda. Mtu mwenye presha ni yule ambaye ana shinikizo la damu la sistoliki linazoanzia 140 milimita za mercury na kuendelea na lile la diastoliki la 90 milimita za mercury na kuendelea. Mahitaji ya huduma ya dharura hutegemea aina ya mgonjwa na endapo anatumia dawa au la.


