top of page

Kamusi Tiba ya ULY CLINIC

Asynergy

Asynergy

Asynergy neno tiba lenye jina la kiswahili la "Asineji" ambapo ni hali ya kitabibu inayohusisha kushindwa kwa misuli au vikundi vya misuli kufanya kazi kwa mpangilio na uratibu unaotarajiwa wakati wa kutekeleza harakati fulani. Katika hali hii, sehemu za mwili ambazo kwa kawaida hufanya kazi kwa pamoja (kwa mfano bega, kiwiko na mkono) hushindwa kushirikiana ipasavyo, na kusababisha harakati zisizo kamilifu, zisizo laini, au zisizo na mfuatano sahihi. Asineji ni dalili ya uharibifu au usumbufu katika maeneo ya ubongo yanayosimamia uratibu wa mwendo.

Ataxia

Ataxia

Ataxia ni neno tiba lenye jina la kiswahili la "Ataksia" ambapo ni hali ya kitabibu inayojitokeza pale ambapo kuna uharibifu au usumbufu katika mfumo wa neva unaodhibiti uratibu wa misuli, hasa serebelamu na miunganisho yake. Hali hii husababisha harakati zisizo sahihi, zisizo na mpangilio, au zisizo thabiti, licha ya nguvu za misuli kuwepo.

Athrosentesisi ni nini?

Athrosentesisi

Ni mchakato wa kitabibu wa kutoa majimaji yaliyokusanyika ndani ya maungio kwa kutumia sindano. Mara nyingi hufanyika kwenye viungo kama goti, kifundo cha mguu, kiwiko au bega ili kuchunguza chanzo cha kuvimba na maumivu ya maungio.

Atopic dermatitis

Atopic Dermatitis

Atopic dermatitis ni neno tiba lenye jina la kiswahili la Ni neno tiba lenye jina la kiswahili la Dermatitisi ya Kiatopiki ni hali ya kitabibu ya muda mrefu (sugu) ya ngozi inayotokana na mchanganyiko wa sababu za kinasaba, kinga ya mwili, na mazingira. Hali hii husababisha kuvurugika kwa kuta ya ulinzi wa ngozi, jambo linalofanya ngozi iwe rahisi kukauka, kuingia vijidudu, na kutoa mwitikio mkali wa mzio.

Atrophic vaginitis ni nini kwa kiswahili?

Atrophic vaginitis

Atrophic vaginitis ni neno tiba lenye jina la kiswahili la Atrofia ya uke ni hali ya kitabibu inayotokea pale ambapo tishu za uke hupungua unene, unyevunyevu, na uimara wake kutokana na upungufu wa homoni ya estrogeni. Hali hii husababisha mabadiliko ya kimuundo na kifizikia katika ukuta wa uke, ikiwa ni pamoja na kukauka, kupungua kwa uwezo wa kutanuka na kusinyaa, na kuongezeka kwa uwezekano wa maumivu au michubuko.

bottom of page