top of page

Kamusi Tiba ya ULY CLINIC

Mafuta yasiyoshamiri

Mafuta yasiyoshamiri

Ni aina ya mafuta yenye molekyuli chache za hydrojeni na huku ikiwa na molekyuli nyingi za tindikali ya mafuta.

Magonjwa ya kuambukiza

Magonjwa ya kuambukiza

Magonjwa ya kuambukiza ni yale yanayosababishwa na vimelea wa aina mbalimbali na huenezwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu/watu wengine wenye vimelea kwa kugusa, kula au kunywa maji, kuvuta hewa, kujamiana n.k

Magonjwa ya moyo baada ya kuzaliwa ni nini?

Magonjwa ya moyo baada ya kuzaliwa

Ni matatizo ya moyo ambayo hutokea baada ya mtu kuzaliwa kutokana na sababu mbalimbali za kiafya au mazingira. Kwa maana hii, yanatofautishwa na magonjwa ya moyo ya kuzaliwa, ambayo mtoto huwa nayo tangu anapozaliwa, na magonjwa ya moyo ya kurithi, ambayo yanahusishwa na mabadiliko ya vinasaba yanayoweza kupitishwa ndani ya familia.

Magonjwa ya moyo ya kuambukiza ni nini?

Magonjwa ya moyo ya kuambukiza

Ni magonjwa ya moyo yanayosababishwa na vijidudu kama bakteria, virusi, fangasi au vimelea wengine. Maambukizi yanaweza kuathiri sehemu mbalimbali za moyo, ikiwemo utando wa ndani wa moyo, misuli ya moyo, utando unaozunguka moyo au valvu za moyo.

Magonjwa ya moyo ya kurithi ni nini?

Magonjwa ya moyo ya kurithi

Ni kundi la magonjwa ya moyo yanayosababishwa au kuchangiwa na mabadiliko katika vinasaba ambayo yanaweza kupitishwa kutoka kwa mzazi kwenda kwa mtoto. Magonjwa haya yanaweza kuathiri misuli ya moyo, mpangilio wa mapigo ya moyo, valvu au jinsi moyo unavyofanya kazi.

bottom of page