top of page

Kamusi Tiba ya ULY CLINIC

Magonjwa ya moyo ya kuzaliwa ni nini?

Magonjwa ya moyo ya kuzaliwa

Ni kundi la matatizo ya muundo au utendaji wa moyo ambayo huwa yapo tangu mtoto anapozaliwa. Matatizo haya yanaweza kuhusisha vyumba vya moyo, valvu, mishipa mikubwa ya damu au namna damu inavyopita ndani na nje ya moyo.

Magonjwa ya moyo yasiyo ya kuambukiza ni nini?

Magonjwa ya moyo yasiyo ya kuambukiza

Ni magonjwa yanayoathiri moyo au mishipa ya damu bila kusababishwa na maambukizi ya bakteria, virusi, fangasi au vimelea wengine. Ni kundi kubwa la magonjwa ya moyo na mishipa ya damu, na yanaweza kutokea kutokana na vinasaba, mtindo wa maisha, umri au magonjwa mengine.

Magonjwa ya mtafunokinga

Magonjwa ya mtafunokinga

Ni magonjwa yatokanayo na shambulio binafsi la kinga ya mwili. Chembe za ulinzi zinazozalishwa huchanganya chembe za mwili na zile za magonjwa na hivyo kupelekea kuziharibu na kuleta dalili mbalimbali.

Magonjwa ya valvu za moyo ni nini?

Magonjwa ya valvu za moyo

Ni matatizo yanayoathiri valvu za moyo, ambazo husaidia kudhibiti mwelekeo wa damu inapopita ndani ya moyo. Valvu zinaweza kushindwa kufunguka vizuri (kubana kwa valvu) au kushindwa kufunga vizuri na kusababisha damu kurudi nyuma (kuvuja kwa valvu).

Magonjwa yasiyo ya kuambukizi

Magonjwa yasiyo ya kuambukiza

Ni magonjwa yanayotokana na mabadiliko katika utendaji kazi wa kawaida wa mwili yanayosababishwa na mabadiliko au mtindo mbaya wa maisha

bottom of page