Mgonjwa wa kisukari anapoumwa, kiwango cha huweza badilika au kubaki kile kile. Wakati huu unashauriwa kupima kiwango cha sukari mara nyingi kuliko kawaida mfano mara tatu hadi nne kwa siku.
Uzito mkubwa, kutoshughulisha mwili, historia ya kisukari kwa ndugu wa damu moja, kisukari cha ujauzito ni miongoni mwa vihatarishi vya kupata kisukari. Unaweza kudhibiti baadhi ya vihatarishi hivi kwa kufanya mazoezi na kuzingatia mlo.