top of page

Mwandishi:

Mhhariri

ULY CLINIC

Dkt. Rachel L, MD

Ijumaa, 5 Novemba 2021

Ulimi kuwaka moto

Ulimi kuwaka moto

Ulimi kuwaka moto ni tatizo la ulimu kuwa na hisia za kuungua na wakati mwingine maumivu huwa makali kama vile umeungua na maji ya moto. Tatizo hili linaweza kuwa la kujirudia au limetokea kwa mara ya kwanza na huweza kuhusisha sehemu mbalimbali za kinywa kama ulimi, fizi, ndani ya mashavu, paa la mdomo na sakafu ya mdomo au mdomo wote.


Dalili


Dalili za ulimu kuwaka moto mbali na hisia za ulimi kuungua huweza kuwa pamoja na;

  • Kuhisi kinywa kimekuwa kikavu au kuwa na kiu sana

  • Kubadilika kwa randha ya chakula, kuhisi kama umekunywa dawa ya metronidazole, yenye radha ya metalik

  • Kupoteza hisia za radha ya chakula

  • Kuwashwa, kuchoma au kufa ganzi kwa ulimi

​

Visababishi

​

Vinaweza kuwa visababishi vya awali au visababishi vinavyotokana na Matatizo fulani mwilini;

Visababishi vya awali huwa mara zote haviambatani na mabadiliko ya kifiziolojia mwilini. Mtu akipimwa, kila kitu huonekana kipo sawa. Tafiti zinaonyesha maumivu haya huenda yakawa yanahusiana na mabadiliko kwenye mishipa ya fahamu.

​

Visababishi vingine huwa ni

​

  • Kinywa kikavu- husababishwa na magonjwa ya kushindwa kuzalisha mate, madawa aina fulani yanayozuia uzalishaji mate au matibabu ya saratani

  • Matatizo mengine ya kinywa- kama maambukizi ya fangas, michomo kwenye ngozi, au tatizo la ulimi ramani au kwa jina jingine ulimi jeografia

  • Upungufu wa viinirishi- Upungufu wa vitamin B12, madini ya zinc,vitamin B9, B1 B2 B6

  • Mzio/aleji- mzio na chakula aina fulani kama vitunza vyakula vya kusindikwa au vyakula vilivyoongezewa ladha isiyo halisi.

  • Tatizo la kucheua- tatizo la kucheua (GERD) husabaisha tindikali ya tumboni kuchoma ulimi na mtu kuhisi hali ya ulimi kuungua.

  • Madawa aina fulani- Madawa ya kushusha shinikizo la damu

  • Mazoea na tabia- tabia ya kutoa uliminje kwa nguvu, kujingata ulimiau, kung’ata meno huweza kuambatana na maatatizo ya ulimi kuwaka moto.

  • Matatizo ya homoni- kama ugonjwa wa kisukari, au upungufu wa homoni ya thyroid

  • Kuchokoza ulimi- kwa kupiga mswaki sana, kutumia dawa za meno zinazounguza, kutumia sana dawa zinazounguza ulimi kama zile za kusafisha ulimi, au kunywa vilevi vyenye tindikali kwa wingi.

  • Matatizo ya kisaikolojia- Mfano msongo wa mawazo, na huzuniko

  • Kuvaa meno bandia ambayo hayakai vema kwenye mdomo huweza kusababisha michomo kwenye ulimina kuhisi hali ya kuungua pia

Vihatarishi

​

Vihatarishi vya kupata tatizo hili la ulimi kuwaka moto ni

  • Hali ya kuwa na ugonwjwa hivi karibuni

  • Magonjwa sugu aina fulani kama ugonjwa wa parkinson’s, magonjwa ya shambulia la kinga za mwili na magonjwa ya mishipaya fahamu

  • Madawa aina fulani

  • Mzio na chakula au dawa aina fulani

  • Huzuniko

  • Kupata majeraha kwenye maisha

​

Mtu anaweza kupata madhara aina fulani akiwa na tatizo hili la ulimi kuwaka moto kama vile kushindwa kulala vema, kushindwa kula chakula, huzuniko na hofu iliyopitiliza.

Kujikinga

​

Hakuna njia ya kujikinga inayojulikana, mtu anaweza kuzuia baadhi ya vihatarishi mfano kuacha kuvuta sigara, kuacha vyakula vyenye tindikali na pilipili kwa wingi na vinywaji nyenye gesi ya carbon kama vile soda na kuepuka msongo wa mawazo.

​

Vipimo na matibabu

​

Vipimo vitahusisha kuchukuliwa historia ya tatizo lako na kuangaliwa ulimi. Daktari anaweza kuagiza vipimo mbalimbali ili kujua visababishi au madhara yaliyojitokeza au kuweza kujitokeza.

Tiba ya kuondoa tatizo kabisa bado haijulikani, hata hivyo tiba dhidi ya dalili zinazojitokeza zipo

​

Matibabu hayo yanahusisha

  • Kupata dawa za kurudisha mate kinywani

  • Dawa za kuosha kinywa

  • Dawa za kuondoa maumivu

  • Dawa za kutibu huzuniko au msongo wa mawazo

  • Matibabu ya kujitambua ili kuondoa hofu iliyopitiliza

​

Matibabu ya nyumbani


  • Kunywa maji ya kutosha, kuzuia tatizo la mdomo mkavu na unaweza kulamba barafu ya vipande vidogo vidogo

  • Zuia kula vyakula vyenye tindikali kwa wingi kama nyanya, juisi ya machungwa, ndimu na vinywaji vyenye gesi ya carbon mfano soda n.k

  • Acha kunywa pombe na vinywaji jamii ya pombe maana huamsha hisia za ulimi wako

  • Usivute sigara wala kutumia tumbaku

  • Jizuie kula vyakula vya moto vyenye viungo vingi

  • Usile vyakula vyenye mdalasini au kemikali ya minti kama pipi na baadhi ya dawa za meno

  • Tumia dawa za meno ambazo hazijawekewa radha

  • Chukua hatua kujikinga na msongo wa mawazo kwa kufanya mazoezi ya yoga, kushiriki michezo au kushirikiana na jamii, usikae mpweke

ULY CLINIC inakushauri siku zote uwasiliane na daktari wako kwa ushauri na tiba kabla ya kuchukua hatua yoyote ya kitiba baada ya kusoma makala hii.

Wasiliana na daktari wa ulyclinic kwa ushauri zaidi na tiba kwa kubofya 'Pata Tiba,  au ''mawasiliano yetu' chini ya tovuti hii

Imeboreshwa,

13 Julai 2023 19:03:14

Rejea za mada hii:

bottom of page