top of page

Dalili na viashiria vya magonjwa mbalimbali

Unashauriwa kufuata ushauri wa daktari wako kabla ya kuchukua hatua yoyote ile baada ya kusoma makala. Bofya picha au neno soma zaidi ili kuingia kwenye makala kwa undani.

Prostatitis

Prostatitis

Ni kuvimba kwa tezi dume kunakosababisha maumivu ya chini ya tumbo, kinena, au rektamu, pamoja na dalili kama kukojoa mara kwa mara na maumivu ya mkojo. Katika hali sugu, inaweza kusababisha maumivu ya korodani, uume, na wakati wa kumwaga mbegu.

Selimundu kali

Selimundu kali

Ni hali ya ghafla inayosababisha maumivu makali ya tumbo, kifua, mgongo, mikono, au miguu, pamoja na udhaifu, maumivu ya viungo, upungufu wa hewa, na manjano kwenye macho.

Shambulio kali la pumu ya kifua

Shambulio kali la pumu ya kifua

Ni hali inayosababisha matumizi makubwa ya misuli saidizi ya kupumua, ikifuatana na shida ya kupumua, miruzi ya kifua, kikohozi, na midomo au kucha kuwa na rangi ya bluu. Katika mashambulizi makali, sauti za kupumua zinaweza kuwa hafifu au kutosikika kabisa.

Embolism ya mapafu

Embolism ya mapafu

Husababisha kupumua kwa shida, haraka, maumivu ya kifua, wasiwasi, na mapigo ya moyo kwenda kasi. Embolus kubwa inaweza kusababishakukohoa damu, ubuluu kwenye ngozi na vidole, kuzimia, na uvimbe wa mishipa ya shingo.

Peritonitisi

Peritonitisi

Husababisha maumivu makali na ukakamavu wa tumbo, dalili nyingine ni homa, kichefuchefu, kutapika, na shinikizo la chini la damu.

bottom of page