top of page

Habari za afya

Soma habari mpya na matukio katika fani za afya kutoka kona mbalimbali za Dunia na Tanzania

Usipuuze Maarifa ya Afya - Shiriki Tafiti hii.

Usipuuze Maarifa ya Afya - Shiriki Tafiti hii.

Tovuti hii imeandaliwa kukupa elimu sahihi ya afya kutoka kwa wataalamu bila gharama. Kuwa miongoni mwa watu 380 wa kwanza kushiriki katika tafiti yetu ya kuboresha upatikanaji wa maarifa ya Afya kwenye tovuti hii kwa kutumia Akili Unde (AI). Bofya linki iliyo kwenye picha hii sasa kushiriki. Ushiriki wako utasaidia kufanya maboresho makubwa na kukidhi mahitaji yako ya kielimu ya afya bila gharama.

Programu ya Mafunzo ya Uandaaji wa Lishe Bora ya Mtoto

Programu ya Mafunzo ya Uandaaji wa Lishe Bora ya Mtoto

Ni muhimu kuchagua nafaka zisizokobolewa, mikunde yenye protini nyingi na mbegu zenye mafuta mazuri kama karanga na mbegu za maboga wakati wa kuandaa unga wa lishe ya mtoto. Malighafi zinapaswa kuwa safi, bila ukungu au wadudu, na ni vyema kuchanganya vyakula vinavyopatikana kirahisi ili mtoto apate virutubishi kamili.

Boresha Afya yako na Jamii kwa kushiriki Utafiti

Boresha Afya yako na Jamii kwa kushiriki Utafiti

Jiunge na ULYCLINIC kushiriki katika utafiti wa Jukwaa la Afya la Akili unde kwa Kiswahili na uchangie kuboresha uelewa wa afya kwa wagonjwa na wahudumu wa afya. Ushiriki wako wa hiari utasaidia kuimarisha huduma za afya na kuchochea maendeleo ya kisayansi kwa kutumia lugha yetu ya Taifa, Kiswahili.

Dawa Mpya zinazobadilisha Matibabu ya Magonjwa Makuu 2025–2026

Dawa Mpya zinazobadilisha Matibabu ya Magonjwa Makuu 2025–2026

Donidalorsen, Plozasiran, Aficamten, Elamipretide, na Ziftomenib (Komzifti) ni dawa mpya za tiba ya uvimbe wa mwili wa kurithi, matatizo ya mafuta mengi kwenye damu, ugonjwa wa kutanuka kwa moyo, ugonjwa wa nishati ya seli, na saratani kali ya damu aina ya mayeloidi leukemia. Ugunduzi wa dawa hizi ni hatua muhimu katika tiba ya kisasa inayolenga sababu za msingi za ugonjwa badala ya dalili tu.

Tahadhari ya Magonjwa ya Milipuko: Influenza, UVIKO-19, Dengue na Kipindupindu

Tahadhari ya Magonjwa ya Milipuko: Influenza, UVIKO-19, Dengue na Kipindupindu

Kwa mujibu wa taarifa ya Mganga Mkuu wa Serikali ya tarehe 25/02/2026, Wizara ya Afya imeonya kuhusu hatari ya kuongezeka kwa maambukizi ya Influenza, UVIKO-19, Dengue na Kipindupindu, hasa katika kipindi cha mvua na mabadiliko ya hali ya hewa. Wananchi wameshauriwa kuzingatia usafi binafsi na wa mazingira, kudhibiti mazalia ya mbu, kutumia maji salama, na kuwahi hospitalini mapema ili kuzuia kusambaa kwa magonjwa haya.

bottom of page