top of page
Kamusi Tiba ya ULY CLINIC

Motor Agraphia
Hufahamika kiswahili kama Agrafia ya misuli, ni aina ya agrafia inayotokea pale ambapo mtu hushindwa kuandika kwa usahihi kutokana na udhaifu wa misuli, kupooza, au matatizo ya neva yanayodhibiti harakati za mkono na vidole. Katika hali hii, mfumo wa lugha huwa haujaathirika; mtu anaweza kufikiri, kuelewa, na kupanga maneno kwa usahihi, lakini hushindwa kuyatekeleza katika maandishi kwa sababu ya changamoto za kimwili.
Msamba (periniamu)
Msamba (periniamu) ni eneo la mwili lililopo kati ya sehemu za siri na njia ya haja kubwa. Kwa mwanamke, msamba huanzia kwenye sehemu ya chini ya mlango wa uke na kuendelea hadi kwenye njia ya haja kubwa. Kwa mwanaume, eneo hili hupatikana kati ya mfuko wa korodani na njia ya haja kubwa.
bottom of page


