top of page

Kamusi Tiba ya ULY CLINIC

aflatoxin, aflatoksin

Sumu ya mazao

Huzalishwa na fangasi jamii ya Aspergillus katika mazao kama mahindi, karanga n.k. utumiaji wa vyakula vyenye sumu hii husababisha kichefuchefu, kutapika, maumivu ya tumbo, degedege na saratani.

TDS kirefu chake ni nini?

TDS katika tiba ni kifupisho cha neno la Kilatin "ter die sumendus" linalomaanisha kutumiwa mara tatu kwa siku. Neno hili hutumika kuamuru dawa ya kunywa itumike mara tatu kwa siku.

Unaweza kutumia pia kama kifupi cha 't.d.s

TID kirefu chake ni nini?

TID ni kifupisho cha neno la Kilatini 'ter in die' linalotumika kwenye tiba na lenye maana ya 'mara tatu kila siku' yaani kila baada ya masaa 8

Takikadia ni nini?

Takikadia

 Ni hali ambapo moyo hupiga kwa kasi zaidi ya kawaida, yaani mapigo ya moyo ya mtu mzima aliyepumzika yanazidi 100 kwa dakika. Takikadia ni jina la kitabibu linalotumika kuelezea mapigo ya moyo kwenda kasi. Kwa kawaida, mapigo ya moyo ya mtu mzima aliyepumzika huwa kati ya 60–100 kwa dakika.

Tamponedi ya moyo ni nini

Tamponedi ya moyo

Ni hali ya hatari ambapo majimaji, damu au vitu vingine hukusanyika ndani ya mfuko unaozunguka moyo (perikadiamu) na kuweka shinikizo kwenye moyo. Shinikizo hilo huzuia moyo kujaza damu vizuri wakati wa mapigo yake, hivyo kiasi cha damu kinachosukumwa kwenda mwilini hupungua.

bottom of page