top of page
Magonjwa na saratani mbalimbali
Sehemu hii utasoma kuhusu hali na magonjwa mbalimbali

Homa ya uti wa mgongo
Watu waishio katika ukanda wa homa ya uti wa mgongo Afrika hupata mlipuko wa homa hiyo kutokana na kuambukizwa kwa njia ya hewa bakteria Neisseria meningitidis. Baadhi ya dalili zake ni homa ya ghafla, maumivu makali ya kichwa, kukakamaa kwa shingo, kichefuchu na kutapika. Ili kutopoteza maisha, fika kituo cha afya karibu nawe kwa tiba ya haraka.
bottom of page



