Vidokezo vya Afya

Syndrome ya Asherman
Asilimia 30 ya wanawake wanaokwanguliwa kizazi ili kutoa mimba yenye miezi mitatu au zaidi, hupata makovu makali ndani ya kizazi yanayosababisha ‘Syndrome ya Asherman’. Watu wenye syndrome hii hupata matatizo ya uzazi kama maumivu makali ya hedhi, kutokuona hedhi, ugumba n.k. Tumia njia za uzazi wa mpango, epuka kupata au kutoa mimba zisizotarajiwa.

Tabia ya kukufanya upate usingizi kwa wakati
Lala na amka muda uleule kila siku, zima taa kutengeneza giza na hakikisha hakuna kelele yoyote, zima na weka simu mbali na kitanda, usile mlo mkubwa wala kunywa kahawa au pombe masaa matatu kabla ya kulala na fanya mazoezi au kazi ya kukutoa jasho wakati wa mchana.

Tovuti salama kwa ushauri wa afya
Kuna zadi ya tovuti 70,000 za afya duniani zinaongezekaa kila kukicha, ni jukumu la mtumiaji kufahamu namna ya kutambua na kutumia vyanzo salama ili kuepuka madhara. Baadhi ya sifa ya chanzo salama ni kuonyesha madhumuni ya tovuti, mada zimeandikwa na kuhaririwa na mtaalamu wa afya na kutoshawishi mtumiaji kununua au kutafuta huduma kutoka kwenye chanzo tu.


