top of page

Vidokezo vya Afya

Usitupe chooni au kuchimbia aridhini dawa zilizoisha muda wa matumizi

Usitupe chooni au kuchimbia aridhini dawa zilizoisha muda wa matumizi

Dawa zilizokwisha muda wake hupaswa kuteketezwa kwa utaratibu maalumu. Endapo umepewa maelekezo ya namna ya kuteketeza dawa zisizotumika, fuata maelekezo hayo kuziteketeza.Endapo hujapewa, zirejeshe kwa mfamasi au hospitali ili zikateketezwe kwa usalama. Usitupe chooni au kuchimbia aridhini, kuepuka madhara ya kiafya.

Usugu wa vimelea vya maradhi kwenye dawa

Usugu wa vimelea vya maradhi kwenye dawa

Matumizi yasiyo sahihi ya dawa jamii ya ‘antibiotic’ na ‘antifungal’ zinazotibu magonjwa mbalimbali kama kisonono, TB, UTI, tonses, nimonia, homa ya matumbo, fangasi ukeni n.k, husababisha vimelea kuwa sugu na kutotibika na dawa hizo. Tumia dawa kama ulivyoandikiwa na daktari wako.

Utambuzi wa VVU ndani ya masaa 24 hadi siku 90

Utambuzi wa VVU ndani ya masaa 24 hadi siku 90

Unaweza kutambulika kwa kipimo kama umepata maambukizi ya VVU ndani ya siku 9 hadi 90 baada ya kupata maambukizi.

Utambuzi wa jinsia ya mtoto tumboni

Utambuzi wa jinsia ya mtoto tumboni

Wajawazito wanaweza kutambua jinsia ya mtoto kupitia DNA-PCR, ultrasound, au CVS, kila moja ikiwa na umri unaopendekezwa na kiwango cha usahihi tofauti. Kufahamu jinsia kunasaidia kupanga maandalizi, kupunguza msongo, na kuimarisha uhusiano wa mama na mtoto tumboni.

Utofauti wa HIV-1 na  HIV-2

Utofauti wa HIV-1 na HIV-2

Kirusi cha HIV1 kilichosambaa duniani kote husababisha UKIMWI kwa haraka ukilinganisha na HIV2 kinachopatikana Afrika magharibi.

bottom of page