top of page

Dalili na viashiria vya magonjwa mbalimbali

Unashauriwa kufuata ushauri wa daktari wako kabla ya kuchukua hatua yoyote ile baada ya kusoma makala. Bofya picha au neno soma zaidi ili kuingia kwenye makala kwa undani.

Maumivu ya tumbo kwa mwanamke (Mitoshimaz)

Maumivu ya tumbo kwa mwanamke (Mitoshimaz)

Mitoshimaz ni neno tiba linalotumiwa na ULY clinic kumaanisha “mittelschmerz”. Mittelschmerz ni neno lililotokana na neno la Kijerumani linalomaanisha “maumivu ya katikati” na kitiba linatumika kumaanisha maumivu ya tumbo upande mmoja wakati wa ovulesheni- yai linalotolewa kutoka kwenye ovari.

Siku ya kupata mimba- Ovulesheni

Siku ya kupata mimba- Ovulesheni

Ovulation ni kitendo cha kutolewa kwa yai kutoka kwenye ovari, yai linapotolewa na ovari husafirishwa kwenda kwenye mji wa mimba(mfuko wa uzazi) kupitia mirija ya fallopio.

Ulimi uliopasuka

Ulimi uliopasuka

Ulimi uliopasuka na kuwa na mifereji (ulimi kuchanika) ni tatizo linalojulikana sana, tatizo hili hutokana na matatizo asili ya kiuumbaji na hakuna kisababishi kinachofahamika kusababisha tatizo hili. Hata hivyo tatizo hili si saratani wala halina hatari ya kuwa saratani.

Kwashiakoo

Kwashiakoo

Utapiamlo ni hali ya kiafya inayosababishwa kwa kula chakula chenye virutubisho vingi au vichache zaidi ya vinavyo takiwa na hivyo kudhuru mwili.

Kutapika

Kutapika

Kutapika ni kitendo cha kutoa nje ya mwili chakula au maji maji yaliyo tumboni kupitia mdomo, kitendo hiki hufanyika kwa haraka na huweza ambatana na maumivu katikati ya kifua.

bottom of page