top of page

Kamusi Tiba ya ULY CLINIC

p.a.a ni kirefu cha nini?

p.a.a. katika tiba na dawa ni kifupisho cha neno la Kilatini ‘parti affectae applicandus’ lenye maana ya ‘paka sehemu iliyoathirika’

p.c kirefu chake ni nini?

p.c katika tiba ni kifupisho cha neno la kilatini "post cibum" lenye maana ya ‘baada ya chakula’. Kwenye cheti cha dawa neno hili linamaanisha tumia dawa baada ya chakula.

p.o kirefu chake ni nini?

p.o ni kifupisho cha neno la Kilatini "per os" lenye maana ya ‘kwa kinywa’. Katika cheti cha dawa, neno hili likitumika humaanisha dawa hiyo itumiwe kupitia kinywa

p.r.n kirefu chake ninini?

p.r.n katika cheti cha dawa na kwenye tiba ni kifupisho cha neno la Kilatini ‘pro re nata' lenye maana ya ‘tumia pale inapolazimu’

Katika cheti cha dawa, kutumia kifupisho p.r.n humaanisha dawa hiyo haijapangiwa muda maalumu wa kutumika, mgonjwa atapaswa kutumia dawa pale endapo anapata dalili tu.

q.d kirefu chake ni nini?

q.d ni kifupisho cha neno la Kilatini ‘quaque die’ lenye maana ya ‘kila siku’

Katika cheti cha dawa au tiba, endapo q.d. itatumika, huashiria kuwa dawa hiyo itumike kila siku.

bottom of page