Maelezo ya majibu ya maswali mbalimbali ya kiafya

Osha na chemsha mayai kujikinga na Taifod
Viumbe jamii ya ndege wenye maambukizi ya kimelea cha ‘salmonella’ kinachosababisha taifodi, huzalisha mayai yenye vimelea hao. Hata hivyo pia yai huweza kubeba vimelea kwa nje endapo litagusa kinyesi chenye vimelea. Osha na chemsha mayai yako kuepuka maambukizi hayo

Mtoto akiwa na homa
Mtoto akiwa na homa ya nyuzi joto za selsiasi 38 au zaidi kwa siku tatu mfululizo, isiyoshuka kwa dawa, au kupata dalili za hatari kama degedege, harara kwenye ngozi, kukakamaa shingo, maumivu ya kichwa, kuharisha, vidonda kooni, maumivu ya sikio, kukataa kula au kunywa, kuwa dhaifu au kutapika. Wasiliana na daktari mara moja.

Kulia machozi huondoa homoni zinazoleta msongo mwilini
Tafiti mbalimbali zinaoyesha kuwa, mtu akilia machozi kutokana na msongo mwilini, machozi yanayotoka hutoa sumu na homoni mbalimbali zinazosababisha msongo mwilini. Homoni za msongo zinapoachiliwa kwenye machozi baada ya kulia husababisha mfumo unaohusika kutuliza mwili ufanye kazi vema na hivyo husababisha kupata tumaini, kufikiria vema na wakati mwingine kupata usingizi mzuri.



