top of page

Maelezo ya majibu ya maswali mbalimbali ya kiafya

Osha na chemsha mayai kujikinga na Taifod

Viumbe jamii ya ndege wenye maambukizi ya kimelea cha ‘salmonella’ kinachosababisha taifodi, huzalisha mayai yenye vimelea hao. Hata hivyo pia yai huweza kubeba vimelea kwa nje endapo litagusa kinyesi chenye vimelea. Osha na chemsha mayai yako kuepuka maambukizi hayo

Mtoto akiwa na homa

Mtoto akiwa na homa ya nyuzi joto za selsiasi 38 au zaidi kwa siku tatu mfululizo, isiyoshuka kwa dawa, au kupata dalili za hatari kama degedege, harara kwenye ngozi, kukakamaa shingo, maumivu ya kichwa, kuharisha, vidonda kooni, maumivu ya sikio, kukataa kula au kunywa, kuwa dhaifu au kutapika. Wasiliana na daktari mara moja.

Majira yenye vichocheo viwili na saratani

Matumizi ya majira yenye vichocheo viwili licha ya kupunguza hatari ya kupata saratani ya ovari na kizazi, huongeza hatari ya kupata saratani ya matiti kwa zaidi ya asilimia 20 na shingo ya kizazi kwa kiasi kidogo.

Ishara maalumu kabla ya kifafa

Baadhi ya watu wenye kifafa hupata ishara za onyo kabla ya degedege, zinazojulikana kama aura. Ishara hizi hujumuisha mabadiliko ya hisia, harufu, kuona, au hali ya kihisia, na huwasaidia kujiandaa kabla ya shambulio.

Kulia machozi huondoa homoni zinazoleta msongo mwilini

Tafiti mbalimbali zinaoyesha kuwa, mtu akilia machozi kutokana na msongo mwilini, machozi yanayotoka hutoa sumu na homoni mbalimbali zinazosababisha msongo mwilini. Homoni za msongo zinapoachiliwa kwenye machozi baada ya kulia husababisha mfumo unaohusika kutuliza mwili ufanye kazi vema na hivyo husababisha kupata tumaini, kufikiria vema na wakati mwingine kupata usingizi mzuri.

Lala muda wa kutosha, imarisha afya yako

Kulala muda wa kutosha huongeza ufanisi wa mwili na akili, pia ni kinga ya magonjwa sugu kama kisukari aina ya 2, magonjwa ya moyo, uzito mkubwa kupita kiasi na sonona. Jali afya yako, lala masaa yanayoshauriwa kiafya kulingana na umri wako.

bottom of page