Mlo kamili kwa mtoto wa Miezi 9 kwa ukuaji wa kawaida
Mtoto wa miezi 9 anahitaji mlo kamili wenye virutubisho muhimu kwa ukuaji wa mwili, ubongo na kinga. Makala hii inaeleza ratiba ya mlo wa wiki kwa kutumia vyakula rahisi vinavyopatikana Afrika ili kusaidia maendeleo bora ya mtoto.
Utapiamlo ni hali ya kupungua au kuzidi kwa virutubishi mwilini inayosababishwa na lishe duni au lishe iliyozidi mahitaji ya mwili. Utapiamlo unaotokea sana Afrika hutokana na lishe duni.
Udumavu ni udhaifu wa ukuaji wa mwili na maendeleo ya ukuaji wa mtoto unaotokea kwa mtoto kutokana na lishe duni, kuugua mara kwa mara na kukosa msisimuo wa kisaikolojia na kijamii.
Kama umejifungua mtoto kwa mara ya kwanza inachukua siku 3 hadi nne ili maziwa yaanze kutoka, lakini kama umejifungua zaidi ya mara moja basi huweza kuchukua siku chache zaidi.
Mbinu mbalimbali zinaweza tumiwa na wazazi ili kumfanya mtoto apende kula kama vile kuheshimu hamu yake ya kula, kumpa chakula kidogo na kumuhusisha kwenye uandalizi wa chakula.