Afya ya Mtoto

Maumivu ya tumbo kwa watoto wachanga (chango)
Maumivu ya tumbo ya chango ni maumivu makali ya tumbo yanayokuja na kuondoka ghafla, mara nyingi husababishwa na mshtuko au kubana kwa misuli ya ndani ya tumbo au utumbo. Kwa Kiswahili pia hujulikana kama koliki, hasa kwa watoto wachanga wanaolia sana kwa sababu ya maumivu ya tumbo.

Namna ya kumlaza kichanga kwa usalama
Kumlaza mtoto mchanga kwa usalama kunahusisha kumlaza chali kwenye kitanda chenye godoro gumu na tambarare bila mito, midoli au vitu vingine vinavyoweza kusababisha hatari ya kukosa hewa endapo vitamfunika. Mazingira tulivu, joto la kawaida na kitanda salama humsaidia mtoto kupata usingizi mzuri na kulinda afya na usalama wake.

Kwa nini Mtoto mchanga hulia sana usiku?
Kichanga hulia sana usiku mara nyingi kutokana na njaa, gesi tumboni, nepi chafu, uchovu au hitaji la faraja kutoka kwa mzazi. Kuelewa sababu hizi na kumtuliza mtoto kwa kunyonyesha, kumbeba au kumweka katika mazingira tulivu kunaweza kusaidia kupunguza kulia na kumsaidia mtoto kulala vizuri.

Kumfanya mtoto abeue baada ya kunyonya
Kumbeusha mtoto baada ya kunyonya humsaidia kutoa hewa iliyomezwa wakati wa kunyonya, hivyo kupunguza kujaa kwa tumbo, gesi na kutapika maziwa. Mzazi anaweza kumsaidia mtoto kubeua kwa kumweka begani, kwenye mapaja, au kifuani huku akimpigapiga mgongoni kwa upole.

Kitovu cha mtoto mchanga: Mwongozo kamili
Kitovu ni kipande cha kiungamwana kinachobaki tumboni kwa mtoto baada ya kuzaliwa. Kwa kawaida hukauka na kudondoka ndani ya wiki 1–2 endapo kinatunzwa kwa usafi na kuachwa kikavu bila msuguano au unyevu. Ikiwa kinatoa harufu kali, usaha, kina wekundu unaoenea, kinaleta maumivu kwa mtoto, kinatoa damu nyingi, au hakijadondoka baada ya wiki 3, wasiliana na daktari mara moja kwa uchunguzi na matibabu sahihi.

Kutokuratibika kwa tendo la kujisaidia kwa kichanga
Ni pale ambapo mtoto chini ya miezi sita anataka kujisaidia lakini mwili wake bado haujajifunza jinsi ya kusukuma kinyesi huku akilegeza njia ya haja kubwa kwa wakati mmoja. Hivyo mtoto hulia, hukaza misuli na kukenya kwa dakika 10–20 au zaidi kabla ya kutoa kinyesi laini na cha kawaida.. Hali hii si ugonjwa na huisha jinsi mtoto anavyokuwa.
