Udumavu ni udhaifu wa ukuaji wa mwili na maendeleo ya ukuaji wa mtoto unaotokea kwa mtoto kutokana na lishe duni, kuugua mara kwa mara na kukosa msisimuo wa kisaikolojia na kijamii.
Kama umejifungua mtoto kwa mara ya kwanza inachukua siku 3 hadi nne ili maziwa yaanze kutoka, lakini kama umejifungua zaidi ya mara moja basi huweza kuchukua siku chache zaidi.
Mbinu mbalimbali zinaweza tumiwa na wazazi ili kumfanya mtoto apende kula kama vile kuheshimu hamu yake ya kula, kumpa chakula kidogo na kumuhusisha kwenye uandalizi wa chakula.
Hujitegemea zaidi na huanza kufahamu zaidi kuhusu ndugu na watoto walio nje ya familia. Huwa na muda mwingi wa kuuliza maswali na kutaka fahamu zaidi kuhusu vitu vinavyo mzunguka.
Kipindi hiki mtoto huwa na shauku ya kuwa huru, huwa na fikra kubwa, hupata mabadiliko ya kijamii kihisia na kitabia na huweza kushika maagizo mawili hadi matatu.