Dalili na viashiria vya magonjwa mbalimbali
Unashauriwa kufuata ushauri wa daktari wako kabla ya kuchukua hatua yoyote ile baada ya kusoma makala. Bofya picha au neno soma zaidi ili kuingia kwenye makala kwa undani.

Funza kwenye ngozi
Myiasis ni tatizo linalotokea endapo ngozi imevamiwa na funza wa nzi. kuna wa aina tofauti tofauti za funza wa nzi wanaoweza kuvamia ngozi, hata hivyo funza wa nzi ambao wanavamia mara nyingi ngozi ya binadamu huitwa Dermatobia hominis (botfly wa binadamu) na Cordylobia anthropophaga (tumbu fly)

Kuharisha kinyesi cheusi
Kuharisha hutokea endapo kinyesi hakichatengenezwa vema ndani ya utumbo, hii hutokea kama maji hayajafyonzwa kwa kiwango cha kutosha katika mfumo wa utumbo mpana na hivyo kusababisha kutoa kinyesi kilaini zaidi kwa jina la uharo. Sababu mbalimbali zinaweza kupelekea kuharisha (zisome katika makala ya kuharisha). Katika makala hii utajifunza sababu za kuharisha kinyesi chenye rangi nyeusi.



