top of page

Dalili na viashiria vya magonjwa mbalimbali

Unashauriwa kufuata ushauri wa daktari wako kabla ya kuchukua hatua yoyote ile baada ya kusoma makala. Bofya picha au neno soma zaidi ili kuingia kwenye makala kwa undani.

Vipele ndani ya kope za macho: Visababishi, Uchunguzi, Matibabu na Kinga

Vipele ndani ya kope za macho: Visababishi, Uchunguzi, Matibabu na Kinga

Vipele ndani ya kope za macho husababishwa na kuziba kwa mirija ya mafuta, na huweza kuambatana na maumivu, macho kutoa machozi, au kuathiriwa na mwanga. Mara nyingi hupotea vyenyewe, lakini matibabu ya nyumbani au ushauri wa daktari unaweza kuhitajika endapo haviponi.

Vidonda mdomoni

Vidonda mdomoni

Vidonda mdomoni (aphthous ulcers) ni majeraha yasiyoambukiza yanayojitokeza ndani ya kinywa, mara nyingi huchochewa na vyakula, msongo au upungufu wa virutubishi. Hupotea ndani ya wiki 1–2, lakini vidonda vinavyorudia mara kwa mara vinaweza kuhitaji tiba maalum na uchunguzi wa daktari.

Komahedhi

Komahedhi

Mwanamke mwenye umri kati ya miaka 45 hadi 55 huwa kwenye koma hedhi kama ameacha kuona damu ya mwezi kwa kipindi cha miezi 12 mfululizo, pasipo kuwa na ujauzito au magonjwa yanayoathiri hedhi. Ukiingia koma hedhi kabla ya umri wa miaka 40, wasiliana na daktari kwa uchunguzi na tiba.

Nyuropathi ya pembezoni

Nyuropathi ya pembezoni

Ugonjwa wa neva ni matokeo ya kujeruhiwa kwa ubongo na uti wa mgongo. Majeruhi husababisha udhaifu wa neva, ganzi na maumivu hasa kwenye miishio ya mwili kama vile mikononi na miguuni hata hivyo pia sehemu mbalimbali za mwili huweza kuathiriwa.

Jicho jekundu

Jicho jekundu

Jicho jekundu ni hali inayotokana na kuvimba au maambukizi ya sehemu nyeupe ya jicho, na linaweza kuambatana na maumivu, muwasho au machozi. Tiba hutegemea chanzo chake, na ni muhimu kumuona daktari ikiwa kuna maumivu makali au upofu wa ghafla.

bottom of page