top of page

Dalili na viashiria vya magonjwa mbalimbali

Unashauriwa kufuata ushauri wa daktari wako kabla ya kuchukua hatua yoyote ile baada ya kusoma makala. Bofya picha au neno soma zaidi ili kuingia kwenye makala kwa undani.

Kupoteza uzito

Kupoteza uzito

Kupungua uzito katika tiba na afya ya mwili huchangiwa kiujumla kwa kupungua kwa maji, tishu za adipozi, misuli, madini, tendoni na tishu za konectivu mwilini.

Dalili za matumizi ya dawa za kulevya

Dalili za matumizi ya dawa za kulevya

Madawa ya kulevya ni aina mbalimbali za dawa ambazo huweza kuathiri akili na tabia ya mtu. Mara nyingi watu hawa hujiingiza katika ulevi ambao huwa ni mgumu kuacha kutokana na hali ya kuuzoesha mwili kuishi na madawa haya kila siku.

Kuishiwa pumzi

Kuishiwa pumzi

Hali na magonjwa mbalimbali yanaweza kusababisha tatizo la kuishiwa pumzi. Mara nyingi kuishiwa pumzi hutokana na matatizo ya moyo na mapafu, moyo na mapafu huhusika kwenye uchukuaji na usafirishaji wa hewa safi ya oksijeni kwenda kwenye tishu mbalimbali na kuondoa hewa chafu ya kaboni monoksaidi kwenye damu.

Homon Imbalance: Dalili, Visabaishi, Uchunguzi na Tiba

Homon Imbalance: Dalili, Visabaishi, Uchunguzi na Tiba

Mvurugiko wa homoni unaweza kusababishwa na hali kama matatizo ya tezi ya shingo, ugonjwa wa polisistiki ovari, kisukari, msongo wa mawazo wa muda mrefu, uzito kupita kiasi, baadhi ya dawa na mabadiliko ya kawaida kama ujauzito au komahedhi. Kudhibiti uzito, kula mlo kamili, kufanya mazoezi, kupunguza msongo wa mawazo na kupata uchunguzi wa kitaalamu pale dalili zinapoendelea husaidia kurekebisha uwiano wa homoni na kulinda afya kwa ujumla.

Dalili ya mzio

Dalili ya mzio

Mzio hutokea wakati mfumo wa kinga za mwili unaitikia vitu vigeni vyote vinapoingia kwenye mwili, mfano sumu mbalimbali, harufu za maua na poleni au baadhi ya vyakula kwa baadhi ya watu. Mfumo huu wa kinga za mwili ni muhimu sana kwani husaidia kumlinda mtu na sumu/kemikali ambazo hazihitajiki mwilini.

bottom of page