Vidokezo vya Afya

Maji na mafuta ni miongoni mwa tiba ya kupasuka midomo
Kupasuka midomo ni tatizo linalowapata watu wengi kwa nyakati mbalimbali ndani ya mwaka. Visababishi vinaweza kuwa hali ya hewa ya baridi au yenye ukavu, kuungua na mwanga wa jua, kupulizwa na upepo mkali, kulamba midomo na kupumua kupitia mdomo. Kunywa maji ya kutosha, paka mafuta au 'lip balm' na kujifunika midomo huwa ni tiba pia kinga.

Maji ya bamia huchochea uponyaji wa vidonda vya tumbo
Ukuta wa ndani ya tumbo kwa kawaida umefunikwa kwa ute ute wa mlenda unaozuia kuta za chini zisiunguzwe na tindikali zinazozalishwa tumboni. Kwa mtu mwenye vidonda vya tumbo, ute huu huwa dhaifu na udhaifu husambaa eneo kubwa zaidi. Matumizi ya maji ya bamia hurejesha kuta hii na kuharakisha uponyaji utokee.

Majibu chanya ya VVU pasipo VVU
Majibu chanya ya kipimo cha HIV SD bioline licha ya kushuku maambukizi ya VVU, huweza kuwa chanya kwa mwenye kaswende, kichocho, minyoo, shambulio binafsi la kinga, ujauzito n.k. Majibu chanya yanapaswa kuthibitishwa kwa kipimo cha HIV Uni-Gold au vingine vyenye ufanisi zaidi.


