top of page
Vidokezo vya Afya

Viungo vya chakula kwa mjamzito
Viungo vingi vya chakula ni salama kwa mama mjamzito kama vitatumika kwa kiasi, hata hivyo baadhi yake pia huweza anzisha uchungu, kutoa mimba na madhaifu kwa mtoto. Baadhi ya viungo vya kuepuka au kutumiwa kwa kiasi kidogo sana ni vitunguu swaumu, mbegu za ufuta, uwatu na mdalasini.

Vyakula vinavyochochea tezi pituitari
Pituitari ni tezi inayofanya kazi ya awali kudhibiti ukuaji wa viumbe. Ili kuongeza kasi ya ukuaji kwa njia asili, tumia vyakula vinavyochochea ufanyaji kazi wake kama vile vyenye vitamin D, E na madini manganese mfano nyama, samaki, mayai, karanga, mboga za majani na nafaka zisizokobolewa.
bottom of page



