top of page

Vidokezo vya Afya

Viungo vya chakula kwa mjamzito

Viungo vya chakula kwa mjamzito

Viungo vingi vya chakula ni salama kwa mama mjamzito kama vitatumika kwa kiasi, hata hivyo baadhi yake pia huweza anzisha uchungu, kutoa mimba na madhaifu kwa mtoto. Baadhi ya viungo vya kuepuka au kutumiwa kwa kiasi kidogo sana ni vitunguu swaumu, mbegu za ufuta, uwatu na mdalasini.

Vyakula tofauti na maziwa kwa kichanga

Vyakula tofauti na maziwa kwa kichanga

Vyakula tofauti na maziwa ya mama husababisha majeraha katika mfumo wa chakula wa kichanga yanayoweza kupelekea magonjwa ya kuharisha. Mnyonyeshe mtoto kwa miezi sita ya kwanza kumkinga.

Vyakula vinavyochochea tezi pituitari

Vyakula vinavyochochea tezi pituitari

Pituitari ni tezi inayofanya kazi ya awali kudhibiti ukuaji wa viumbe. Ili kuongeza kasi ya ukuaji kwa njia asili, tumia vyakula vinavyochochea ufanyaji kazi wake kama vile vyenye vitamin D, E na madini manganese mfano nyama, samaki, mayai, karanga, mboga za majani na nafaka zisizokobolewa.

Vyakula vyenye uwezo wa kukupa usingizi

Vyakula vyenye uwezo wa kukupa usingizi

Matumizi ya chai ya maua ya pasheni au chamomile, juisi ya tunda damu au kiwi, karanga ya lozi au jozi na nyama ya bata mzinga huchochea kupata usingizi kwa haraka. Endapo una tatizo la kukosa usingizi, tumia moja ya vitu hivyo.

Wastani wa kufa baada ya miaka 10 kwa mwenye VVU

Wastani wa kufa baada ya miaka 10 kwa mwenye VVU

Wastani wa kufa miaka 10 ijayo kutokana na VVU huongezeka sambamba na idadi ya nakala za virusi kwenye damu miezi sita baada ya kuanza ARV. Kuanza ARV mapema na kuitumia kwa usahihi hupunguza idadi ya nakala za virusi na kuongeza wastani wa kuishi.

bottom of page