top of page

Vidokezo vya Afya

Dawa na virutubisho vinavyotibu COVID-19

Dawa na virutubisho vinavyotibu COVID-19

Tafiti zinaonyesha, dawa azithromycin, madini ya zinc, vitamini C na D na dexamethasone huwa na uwezo wa kukukinga na kutibu magonjwa ya mfumo wa upumuaji kama COVID-19 . Unashauriwa kupata vitamini C na D na madini ya zinc kutoka kwenye vyakula, endapo unahitaji dawa wasiliana na daktari wako.

Degedege kwa kichanga

Degedege kwa kichanga

Mtoto mchanga kupata degedege ni dalili ya kupungua kwa kiwango cha sukari mwilini. Mkinge mwanao kwa kumnyonyeshe dakika 15 hadi 20 angalau mara nane kwa siku.

Epuka chumvi ya kuongezea

Epuka chumvi ya kuongezea

Epuka chumvi: Ili uwe na shinikizo la kawaida la damu, usiongeze chumvi kwenye chakula, weka kidogo unapopika, au achana nayo kabisa, na utaizoea hali hiyo.

Epuka kula chumvi nyingi

Epuka kula chumvi nyingi

Kula chumvi nyingi kila siku huongeza hatari ya kupata shinikizo la juu la damu na kiharusi, hivyo ni muhimu kujihadhari kwa kupunguza chumvi kwenye chakula pamoja na kuepuka vyakula vya kukaangwa na vyakula vilivyosindikwa kama vibanzi na soseji. Badala ya kuongeza chumvi, tumia viungo vya asili kama limao, kitunguu saumu, tangawizi au majani ya chai ili kuboresha ladha ya chakula bila kuongeza hatari kiafya.

Epuka unene

Epuka unene

Epuka kunenepa: Unene huongeza hatari ya magonjwa ya moyo. Kula vyakula visivyo na mafuta mengi, matunda na mboga za majani, na fanya mazoezi upunguze unene.

bottom of page