Hujitegemea zaidi na huanza kufahamu zaidi kuhusu ndugu na watoto walio nje ya familia. Huwa na muda mwingi wa kuuliza maswali na kutaka fahamu zaidi kuhusu vitu vinavyo mzunguka.
Kipindi hiki mtoto huwa na shauku ya kuwa huru, huwa na fikra kubwa, hupata mabadiliko ya kijamii kihisia na kitabia na huweza kushika maagizo mawili hadi matatu.
Kwenye kipindi hiki mtoto anakuwa na tabia ya ubishi na asiyesikia mtu, hujitambua kwenye picha na kioo pia huiga tabia za watu wazima au watoto waliomzidi umri.
Wazazi wengi wanaweza kuandaa lishe ya watoto, lakini changamoto iliyopo ni kwamba hawajui wanatakiwa wawe na vitu gani vya msingi na kwa kiasi gani mchanganyiko unaotakiwa uwe.
Chanjo za watoto hutolewa katika vipindi mbalimbali mtoto anapozaliwa.chanjo hizi hutolewa kwa malemgo ya kumkinga mtoto na magonjwa mbalimbali yanayoweza kutisia uhai Wa mtoto.