Mbinu mbalimbali zinaweza tumiwa na wazazi ili kumfanya mtoto apende kula kama vile kuheshimu hamu yake ya kula, kumpa chakula kidogo na kumuhusisha kwenye uandalizi wa chakula.
Hujitegemea zaidi na huanza kufahamu zaidi kuhusu ndugu na watoto walio nje ya familia. Huwa na muda mwingi wa kuuliza maswali na kutaka fahamu zaidi kuhusu vitu vinavyo mzunguka.
Kipindi hiki mtoto huwa na shauku ya kuwa huru, huwa na fikra kubwa, hupata mabadiliko ya kijamii kihisia na kitabia na huweza kushika maagizo mawili hadi matatu.
Kwenye kipindi hiki mtoto anakuwa na tabia ya ubishi na asiyesikia mtu, hujitambua kwenye picha na kioo pia huiga tabia za watu wazima au watoto waliomzidi umri.