Mwandishi:
Dkt. Sospeter M, MD
Mhariri:
Dkt. Lugonda B, MD
Imeboreshwa:
23 Januari 2026, 14:03:50

Dawa Diclofenac
Ni dawa ya kutibu maumivu jamii ya NSAID’s, hupatikana kwa mfumo wa Kidonge kilichoungwa na madini ya Potasiamu. Kidonge kinaweza kuwa na chenye miligramu 50, 25, 75, 100
Tembe za miligramu 18, 25 na 35
Unga , miligramu 37.5 kwa kila mililita moja ya maji
Jeli au krimu ya kupaka
Rangi ya kidonge
Kidonge cha diclofenac(diklofenaki) kinaweza kuwa cha rangi aina tofauti kama brauni, nyeupe, njano, pinki n.k
Majina mengine ya dawa hii
Cataflam, Voltaren-XR, Dyloject, Cambia, Zipsor, Zorvolex, Diclopa, Declofenac
Matumizi
Kutibu athraitis ya ryumatoid (baridi yabisi)
Osteoathraitiz
Spondilaitiz ya ankailozing
Maumivu ya kiasi hadi wastani
Maudhi ya dawa hii
Kuvimba kwa tumbo na kujamba
Maumivu ya tumbo na Maumivu ya kukata kwa tumbo
Haja ngumu
Kuharisha
Kuvimba
Vidonda vya tumbo na kutokwa damu tumboni
Upele
Masikio kupiga kelele(tinitas)
Hepataitis ya ghafla
Agranulosaitosis
Anemia ya aplastiki
Hepataitis isiyo na dalili
Kupanda kwa kiwango cha BUN zaidiya 40 kwa kila desilita moja
Kolestaisi
Hepatitis sugu
Kupungua kwa hemoglobin
Hepataitis ya kuua ya fulminat
Anemia ya hemolitiki
Nekrosis ya hepatoselula
Manjano
Liukopeni
Sumu kwa figo
Kupandisha kiwango cha creatinine Zaidi ya miligramu 2 kwa kila desilita moja (2mg/dL)
Thrombosaitopenia
Tahadhari
Kwenye mfumo wa moyo
Dawa jamii ya NSAID’s huweza kuongeza hali ya magonjwa hatari ya moyo na matukio ya thrombotiki, infakisheni ya mayokadia, kiharusi, haya yote huweza kuua mtu.
Hatari huongezeka zaidi kulingana na muda wa matumizi
Wagonjwa walio na ugonjwa wa moyo au wenye kihatarishi cha ugonjwa wa moyo wapo hatarini zaidi
NSAID’s haziruhusiwi kutumika wakati wa upasuaji wa mishipa ya damu ya koronari(CABG)
Kwenye mfumo wa chakula
Dawa jamii ya NSAID’s huweza kuongeza hatari ya kutokwa damu tumboni, vidonda vya tumbo na kutoboa utumbo na tumbo ambapo mtu huweza kupoteza Maisha.
Madhara kwenye mfumo huu huweza kutokea ghafla bila ishara
Wazee wapo hatarini kupata madhara mabaya kwenye mfumo huu wa chakula.
Katazo
Marufuku: kutumika kwa watu weye mzio na dawa hii, wenye historia ya kupata madhara ya aspirini, kutibu wagonjwa waliofanyiwa au wanaotaka kufanyiwa upasuaji wa mishipa ya damu ya moyo ya koronari na wale wanaotokwa damu kwenye mfumo wa chakula.
Kwa wagonjwa walioferi figo kwa wastani au kabisa kipindi cha upasuaji, au wagonjwa wenye hatari ya kuishiwa damu.
Watu wenye historia ya mzio na protini ya bovin
Angalizo
Tumia dawa hii kwa umakini kwa wagonjwa hawa
Wenye bronkospazimu
Magonjwa ya moyo
Pofria ya hepatiki
Kuvuta sigara
Lupasi ya erizimatazi kwenye mfumo wa mwili
Thrombosaitoopenia
Kuferi kwa urojo wa mifupa
Agranulosaitosis
Anemia ya Aplastiki
Moyo ulioferi- NSAID’s huweza kusabaisha moyo kuferi kwa kutunza maji na chumvu na mwili kushindwa kuitikia dhidi ya dawa za kuchuja maji.
Matumizi ya diclofenac wakati wa Ujauzito na kunyonyesha
Matumizi ya dawa jamii ya NSAID’swakati wa ujauzito huweza kusababisha kufunga kwa arteriosus ya daktasi kabla ya wakati. Dawa hii inatakiwa kuacha kutumia endapo mimba ina wiki 30 na kuendelea.
Ugumba
Kutokana na ufanyajikazi wake, matumizi ya dawa za NSAID’s zinazofanya kazi na njia ya prostaglandins huweza kuchelewesha kutolewa kwa yai kwenye ovari, hii husababisha ugumba wa muda kwa wanawake. Tafiti kwa Wanyama na binadamu zimeonyesha pia kuchelewa kwa kutolewa kwa mayai kwa kutoka kwenye ovari. Hivyo kwa wanawake ambayo wanafanyiwa vipimo vya ugumba au kutaka Watoto wanaweza kufikiriwa kuacha tumia dawa hii kipindi hiki.
Matumizi ya Diclofenac wakati wa kunyonyesha
Tafiti zinaonekana kuwa kiwango kidogo cha diclofenac hupita na kuingia kwenye maziwa ya mama, lakini hakuna tafiti zinazoonyesha madhara kwa mtoto kutokana na kunyonya maziwa ya mama au madhara dhidi ya uzalishaji wa maziwa. Unapotoa dawah ii hakikisha kuwa faida ni kubwa kuliko madhara yanayoweza kujitokeza kwa mama au mtoto.
Endapo umesahau kunywa dozi
Kama umesahau kunywa dozi yako, unaweza kunywa mara tu unapokumbuka, isipokuwa endapo muda wa dozi ingine umeshafika unatakiwa kuruka hiyo dozi uliyosahau na kuendelea na dozi yako kama muda uliopangiwa.
ONYO: Usitumie dawa yoyote bila ushauri wa daktari. Dawa zinaweza kuleta madhara mwilini na pia matumizi ya baadhi ya dawa pasipo ushauri na vipimo husababisha vimelea kuwa sugu dhidi ya dawa hiyo.
ULY clinic inakushauri kuwasiliana na daktari wako unapotaka kuchukua maamuzi yoyote yanayohusu afya yako.
Wasiliana na daktari/Mfamasia wa ULY clinic kwa ushauri na Tiba au kuandikiwa dawa kwa kupiga simu au Kubonyeza Pata tiba chini ya tovuti hii.
Imeandikwa:
23 Januari 2026, 14:03:50
Rejea za mada hii:-
