top of page

Dawa

ULY CLINIC inakutahadharisha kuwa matumizi ya dawa pasipo ushauri wa daktari yanaweza kuleta madhara makubwa mwilini mwako.

 

Siku zote wasiliana na daktari wako kwa elimu na ushauri wa dawa gani na namna ya kutumia dawa inayoendana na hali yako halisi kama mbadala ya kujichukulia hatua mwenyewe.

Bonyeza 'Soma zaidi ' kwenye dawa unayohitaji kuanza kusoma kuhusu dawa hiyo..

Dawa Pamidronate

Dawa Pamidronate

Pamidronic acid ni dawa ya kizazi cha pili cha bisphosphonate inayotumika katika matibabu ya ugonjwa wa Paget, kushusha kiwango cha juu cha kalisiamu kwenye damu kinachotokana na saratani na mifupa dhaifu.

Dawa Alendronate

Dawa Alendronate

Alendronate ni moja kati ya dawa jamii ya bisphosphonate inayotumika kukinga na kutibu magonjwa ya mifuta dhaifu (yenye hatari ya kuvunjika haraka).

Dawa Etidronate

Dawa Etidronate

Etidronate ni moja kati jamii ya bisphosphonate inayotumika kutibu kukinga na kutibu magonjwa ya magonjwa ya mifupa kama ugonjwa wa paget unaosababisha mifupa kuwa dhaifu na kuvunjika.

Dawa Cycloserine

Dawa Cycloserine

Cycloserine ni moja kati ya antibiotiki katika kundi la antitubakula inayotumika na dawa zingine katika matibabu ya magonjwa yaliyosugu kwenye dawa zingine kutokana na maambukizi ya bakteria mycobacteria tuberculae kama kifua kikuu kutokana (TB).

Dawa Linezolid

Dawa Linezolid

Linezolid ni moja kati ya antibiotik jamii ya oxazolidinone inayotumika kutibu maambukizi ya bakteria jamii ya gramu chanya wanaodhuriwa na dawa hii.

Dawa Clofazimine

Dawa Clofazimine

Clofazimine ni moja ya antibiotiki jamii ya riminophenazine iliyo kwenye kundi la antitubakula, hutumika pamoja na dawa zingine kutibu ukoma. Hufanya kazi kwa kuua bakteria aina ya mycobacterium leprae.

Dawa Bedaquiline

Dawa Bedaquiline

Bedaquiline ni moja kati ya antibiotic jamii ya Antitubakula inayotumika kutibu maambukizi ya bakteria mycobacteria tuberculae anayesababisha kifua kikuu (TB). Bedaquiline imehifadhiwa kutumika kwa wagonjwa wa kifua kikuu kinachosababishwa na bakteria wenye usugu kwenye dawa zingine za TB.

Dawa Ofloxacin

Dawa Ofloxacin

Ofloxacin ni moja ya antibiotic jamii ya Fluoroquinolone inayotumika kutibu magonjwa yanayotokana na maambukizi ya bakteria wanaodhuriwa na dawa hii kama nimonia, selulaitiz, homa ya njia ya mkojo, prostaitiz, plague na aina kadhaa za maradhi ya kuhara.

Dawa Moxifloxacin

Dawa Moxifloxacin

Moxifloxacin ni anitbayotiki ya jamii ya fluoroquinolone inayotumika kutibu maambukizi ya bakteria wanaodhuruwa na dawa hii kama maambukizi kwenye sainazi, njia za hewa na mapafu.

Dawa Levofloxacin

Dawa Levofloxacin

Levofloxacin ni moja ya antibayotiki jamii ya fluoroquinolone inayotumika kutibu maambukizi ya bakteria wanaodhuriwa na dawa kwenye njia ya hewa, ngozi, mfumo wa mkojo, tezi dume na waliojianika kwenye kimeta na plague.

Dawa Cefepime

Dawa Cefepime

Cefepime ni antibiotiki ya kizazi cha nne cha cephalosporin inayotumika katika matibabu ya magonjwa yanayosababiswha na maambukizi ya bakteria mbalimbali wanaodhuriwa na dawa hii kwenye mapafu, mfumo wa mkojo, via vya uzazi, nogzi n.k.

Dawa Imipenem

Dawa Imipenem

Imipenem ni moja kati ya antibiotiki jamii ya carbapenems yenye uwanja mpana wa kudhuru bakteria inayotumika sana ikiwa imeunganika na cilastatin ili kuongeza muda wa ufanyaji kazi wake na kuzuia madhara yake kwenye figo.

Hujapata dawa unayotafuta?

 

Endapo hujapata dawa unayotafuta andika katika kiboksi kilichoandikwa  "Tafuta chochote hapa...." juu ya kurasa hii na endapo hujapata katika kiboksi hiko basi wasiliana na wafamasia wa ULY CLINIC maelezo zaidi kuhusu dawa.

Wasiliana na daktari wa ULY CLINIC kwa ushauri na tiba kwa kubofya linki ya 'Mawasiliano yetu' au 'Pata tiba' chini ya tovuti hii

bottom of page