top of page

Dawa

ULY CLINIC inakutahadharisha kuwa matumizi ya dawa pasipo ushauri wa daktari yanaweza kuleta madhara makubwa mwilini mwako.

 

Siku zote wasiliana na daktari wako kwa elimu na ushauri wa dawa gani na namna ya kutumia dawa inayoendana na hali yako halisi kama mbadala ya kujichukulia hatua mwenyewe.

Bonyeza 'Soma zaidi ' kwenye dawa unayohitaji kuanza kusoma kuhusu dawa hiyo..

Dawa Pyrazinamide

Dawa Pyrazinamide

Pyrazinamide ni moja kati ya antibiotic inayofanya kazi ya kuzuia ukuaji wa bakteria aina ya mycobacteria tuberculae anayesababisha kifua kikuu (TB).

Dawa Dapsone

Dawa Dapsone

Dapsone ni dawa iliyotengenezwa kutoka kwenye diamino-sulfone yenye uwezo wa kuzuia michomo kutokana na kinga za mwili pamoja na uwezo w akufanya kazi kama antibayotiki. Hutumika awali kwenye matibabu ya ukoma na leprosy ugonjwa wa ngozi wa dermatitis herpetiformis.

Dawa Albendazole

Dawa Albendazole

Ni dawa ya ya kutibu maambukizi ya minyoo iliyo katika kundi la anthelmintic. Dawa hii hutibu maambukizi ya minyoo kwa binadamu kutoka kwa mbwa na nguruwe na pia hufahamika kwa jina jingine la procaine, Albenza, Eskazole na Albendazolum.

Dawa Dicloxacillin

Dawa Dicloxacillin

Ni moja ya antibayotiki kwenye kundi la pili la Penicillin, antibayotiki inayotumika kutibu maambukizi ya bakteria wasiozalisha beta lactam na hufahamika kwa majina mengine kama dycill, dynapen.

Dawa Piperacillin/tazobactam

Dawa Piperacillin/tazobactam

Piperacillin tazobactam ni dawa ya antibayotiki katika kundi la penicillin iliyounganishwa na tazobactam kwa ajili ya kuongeza uwezo wake wa kutibu magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na bakteria haswa wa gramu hasi, na kiasi cha bakteria wa gramu chanya na anaerobiki. Tazobactam inayoongezwa kwenye dawa hii huwa na uwezo wa kuzuia kimeng’enya muhimu cha bakteria chenye jina la β-lactamase.

Dawa Fluticasone

Dawa Fluticasone

Ni dawa aina jamii ya corticosteroid maarufu kwa jina jingine la Clarispray, Xhance na Flonase. Dawa hii ni moja ya dawa zinazotumika kunyunyiza ndani ya pua.

Dawa Piperacillin

Dawa Piperacillin

Piperacillin ni dawa ya antibayotiki katika kundi la ureidopenicillin. Dawa hii hutibu maambukizi ya wastani hadi makali ya bakteria wanaodhurika nayo haswa wale wa gramu chanya na hufahamika kwa majina mengine ya pipracil, hubercilina, piperacillin, pipril.

Dawa Rifampicin

Dawa Rifampicin

Rifampicin ni moja kati ya antibiotic kundi la antitubercular inayotumika kutibu maambukizi ya bakteria aina ya mycobacteria tuberculae kwenye anayesababisha kifua kikuu (TB).

Dawa Ethambutol

Dawa Ethambutol

Ethambutol ni moja kati ya antibiotic katika kundi la antitubercular inayotumika kutibu maambukizi ya bakteria aina ya mycobacteria tuberculae moja wa bakteria anayesabisha kifua kikuu (TB). Ethambutol hufahamika kwa jina jingine kama myambutol

Dawa Chloramphenical

Dawa Chloramphenical

Chloramphenical ni moja kati ya antibiotikiya kutengenezwa inayotumika kutibu maambukizi ya bakteria kwa baadhi ya bakteria waliokuwa sugu kwenye antibiotiki zingine.

Dawa Cloxacillin

Dawa Cloxacillin

Cloxacillin ni moja kati ya antibiotiki katika kundi la ‘Penicillin pinzani kwa Penicillinase’ inayotumika kutibu maambukizi ya bakteria jamii ya gram chanya na wale wanaozalisha kimeng’enya cha beta lactamase.

Dawa Cefotaxime

Dawa Cefotaxime

Cefotaxime ni moja ya antibiotiki ya kizazi cha tatu cha cephalosporin inayotumika kutibu maambukizi mbalimbali ya bakteria mwili. Inatumika kwa bakteria wa gram hasi na gram chanya na ipo katika kundi la tatu la dawa

Hujapata dawa unayotafuta?

 

Endapo hujapata dawa unayotafuta andika katika kiboksi kilichoandikwa  "Tafuta chochote hapa...." juu ya kurasa hii na endapo hujapata katika kiboksi hiko basi wasiliana na wafamasia wa ULY CLINIC maelezo zaidi kuhusu dawa.

Wasiliana na daktari wa ULY CLINIC kwa ushauri na tiba kwa kubofya linki ya 'Mawasiliano yetu' au 'Pata tiba' chini ya tovuti hii

bottom of page